in , , ,

Man City mkao wa kula

Timu ya Manchester City imepalilia vyema safari ya kutwaa ubingwa kwa mara ya pili katika miaka mitatu.

City walibanwa nyumbani kwao na Aston Villa kwa zaidi ya saa nzima, kabla ya Edin Dzeko kuwafyatua kwa mabao mawili ya haraka.

Kocha Manuel Pellegrini alijitahidi kuelekeza vijana wake, huku Paul Lambert upande wa pili akiwachagiza wake, waliofanikiwa kuwa na ngome kali hadi kipindi cha pili katikati.

Bao la Steven Jovetic na Yaya Toure dakika za mwisho yaliwazamisha Villa na kufanya Etihad ilipuke kwa vifijo na hoi hoi.

Ushindi huo umeipandisha City kileleni, wakiwazidi Liverpool kwa pointi mbili na idadi kubwa ya mabao ya kufunga kabla ya mechi za mwisho wikiendi hii.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Suarez mwanasoka bora wa mwaka

Blatter kugombea tena Fifa