in

Mamia ya wanafunzi wajiunga na PSPF

MFUKO wa Pensheni wa PSPF, “umevuna” mamia ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, (Shule ya Biashara), ambao wamejiunga ma mpango wa uchangiaji wa hiari PSPF Supplementary Scheme-PSS wakati wa kongamano lililopewa jina, (Women University Platform), na kufanyika chuoni hapo jijini Dar es Salaam.

Sio tu wanafunzi pekee walijiunga na mpango huo, lakini pia watu maarufu kama vile, Mwanamuziki nyota wa muziki wa Bongo Flava, Vanessa Mdee,na  mpeperushaji wa vipindi vya runinga vinavyohusu masuala ya wanawake, Joyce Kiria ambao walikuwa ni  miongoni mwa wasemaji wakuu kwenye kongamano hilo walijiunga pia.

Balozi wa Mfuko wa Pensehni wa PSPF, ambaye pia ni Mwanamitindo wa Kimataifa anayefanya kazi zake Ulaya na Marekani, Flaviana Matata, akiwaeleza wanafunzi wa mwaka wa mwisho wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, (Shule ya Biashara), jinsi ya kutumia vipaji vyao katika kujitengenezea ajira ikiwa ni pamoja na umuhimu wa kujiunga na Mfuko wa PSPF.
Balozi wa Mfuko wa Pensehni wa PSPF, ambaye pia ni Mwanamitindo wa Kimataifa anayefanya kazi zake Ulaya na Marekani, Flaviana Matata, akiwaeleza wanafunzi wa mwaka wa mwisho wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, (Shule ya Biashara), jinsi ya kutumia vipaji vyao katika kujitengenezea ajira ikiwa ni pamoja na umuhimu wa kujiunga na Mfuko wa PSPF.

Kujiunga kwa wanafunzi hao kwenye mpango wa PSS, kulifuatiwa na mfululizo wa elimu ya huduma zitolewazo na Mfuko huo yaliyotolewa na Afisa a Operesheni wa PSPF, Hadji Jamadary, afisa matekelezo, Albert Feruzi, wakiongozwa na Meneja wa mpango huo, yaani PSS, Mwanjaa Sembe, na Balzoi wa PSPF, Mwnaamitindo “nguli” wa Kimataifa anayefanya kazi zake Ulaya na Marekani, Flaviana Matata.

Maafisa wa Mfuko huo, Rahma Ngassa, Gasper Lyimo na wengineo, walilazimika kufanya kazi ya ziada, kuwasaidia wanafunzi hao kujaza fomu hizo na kuchukua picha zao tayari kuwatengenezea vitambulisho.

Afisa wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Delphin Richard, akizungumza kwenye kongamano la wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Tumaini (tawi la Dar es salaam)
Afisa wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Delphin Richard, akizungumza kwenye kongamano la wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Tumaini (tawi la Dar es salaam)

Mambo yaliyowavutia wanafunzi hao na kuamua kujiunga na mpango huo ni zile faida wanazopata wanachama wa PSPF, kama vile Fao la mikopo ya elimu, jipange kimaisha, fao la uzazi, afya, na mikopo ya nyumba na viwanja.

Kongamano hilo lilitanguliwa na kongamano kama hilo lililofanyika Chuo Kikuu Cha Tumaini (tawi la Dar es Salaam, ambapo kazi kama hiyo ilifaywa na Mhamasishaji Anthony Luvanda, kutoka kampuni ya Home of Events, Afisa Masoko Mwandamizi, wa PSPF, Magire Werema, Rahma Ngassa, Delphin Richard, Gasper Lyimo na Balozi wa PSPF, Mrisho Mpoto.

Afisa Masoko mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Magire Werema, (kushoto), akitoa mada kuhusu huduma zitolewazo na Mfuko huo na faida mbalimbali ambazo mwanachama anaweza kuzipata wakati wa kongamano la kutambua fursa lililowaleta pamoja wanafunzi wa mwaka wa mwisho wa Chuo Kikuu Cha Tumaini (tawi la Dar es Salaam). Magire aliwaambia wanafunzi hao kuwa wanachama wa PSPF ni pamoja na Watumishi wa sekta ya Umma, Binafsi, na watu wote walio katika Sekta isiyo Rasmi, (Wajasiriamali). Na kwamba Mwanachama anaweza kufaidika na mafao mbalimbali yatolewayo na Mfuko kama vile mikopo ya elimu, bima ya afya, fao la uzazi, mikopo ya nyumba na viwanja na lile la jipange kimaisha.
Afisa Masoko mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Magire Werema, (kushoto), akitoa mada kuhusu huduma zitolewazo na Mfuko huo na faida mbalimbali ambazo mwanachama anaweza kuzipata wakati wa kongamano la kutambua fursa lililowaleta pamoja wanafunzi wa mwaka wa mwisho wa Chuo Kikuu Cha Tumaini (tawi la Dar es Salaam). Magire aliwaambia wanafunzi hao kuwa wanachama wa PSPF ni pamoja na Watumishi wa sekta ya Umma, Binafsi, na watu wote walio katika Sekta isiyo Rasmi, (Wajasiriamali). Na kwamba Mwanachama anaweza kufaidika na mafao mbalimbali yatolewayo na Mfuko kama vile mikopo ya elimu, bima ya afya, fao la uzazi, mikopo ya nyumba na viwanja na lile la jipange kimaisha.

———————————

Mpeperushaji wa vipindi vya wanawake kwenye runinga, Joyce Kiria, (kushoto), akielekzwa namna ya kujaza fomu za kujiunga na Mpango wa Uchagiaji wa Hiari (PSS), wa Mfuko wa Pensehni wa PSPF, na Balozi wa Mfuko huo, Flaviana Matata
Mpeperushaji wa vipindi vya wanawake kwenye runinga, Joyce Kiria, (kushoto), akielekzwa namna ya kujaza fomu za kujiunga na Mpango wa Uchagiaji wa Hiari (PSS), wa Mfuko wa Pensehni wa PSPF, na Balozi wa Mfuko huo, Flaviana Matata

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

RAUNDI YA TANO KOMBE LA FA:

Tanzania Sports

Guardiola huyoo Man City