in , ,

Majanga Tottenham Hotspur


*West Ham wawanyuka Kombe la Ligi
*Man United nao waingia nusu fainali

Maisha bado ni magumu White Hart Lane, kwani hata baada ya kumfukuza Andre Villas-Boas, Tottenham Hotspur wameendelea kuwa majangani.

Usiku wa Jumatano hii wamejikuta katika wakati mgumu, wakikumbukia kikombe cha mwisho, bila kujali kidogo namna gani, walichokipata 1980.

Spurs walitangulia kufunga bao kupitia kwa Emmanuel Adebayor aliyerejeshwa kikosini sambamba na Jermain Defoe kuwaweka pembeni ‘maswahiba’ wa AVB, lakini timu haikuweza kushikilia bao hilo la dakika ya 67.

West Ham wanaonolewa na Sam Allardyce walisawazisha bao hilo kupitia kwa Matt Jarvis kabla ya kijan Modibo Maliga kupachika bao la ushindi dakika chache tu kabla ya kipenga cha mwisho.

Wachezaji wa Spurs pamoja na mwenyekiti wao, David Levy walionekana kutoamini kilichotokea, lakini ndio hivyo, West Ham wamewang’oa kwenye michuano ya Kombe la Ligi.

Katika mechi nyingine, Manchester United waliwafunga Stoke 2-0 kwa mabao yaliyofungwa na Ashley Young na Patrice Evra, lakini mambo hayakuwa marahisi, kwani United walienda hadi kipindi cha pili.

Kutokana na matokeo hayo, nusu fainali itakuwa baina ya Manchester City na Sunderland wakati Manchester United atakabiliana na West Ham baadaye mwezi ujao wa Januari.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Chelsea watibuliwa na Sunderland

Simba, Yanga meet in derby