Arsenal wamepoteza mechi nyingine kwa kufungwa na Stoke 3-2 katika mechi iliyoanza vibaya kwao, kwani hadi nusu ya kwanza walikuwa chini kwa mabao 3-0.
Wakicheza ugenini, Arsenal walikuwa kama wameloa hadi nusu ya kwanza na walipata pigo zaidi baadaye kwa beki wao chipukizi Calum Chambers kupewa kadi nyekundu. Mabao ya wenyeji yalifungwa na Peter Crouch sekunde ya 19 tu, Bojan akatia la pili na Jon Walters akawaliza kwa la tatu.

Arsenal walirudi vyema kipindi cha pili lakini jitihada zao hazikutosha, kwani walipata mabao mawili kupitia kwa Santi Cazorla na Aaron Ramsey. Dakika 45 za kwanza zilikuwa mbaya zaidi kwa Kocha Arsenal Wenger.

Kwenye mechi nyingine Manchester City walifanikiwa kupata ushindi mwembamba dhidi ya Everton na kupunguza pengo kwa vinara wa ligi, Chelsea, kwa pointi tatu, ambapo bao la City lilifungwa na Yaya Toure kwa penati.

Matokeo mengine ni kwamba Hull walikwenda suluhu na West Bromwich Albion kama ilivyokuwa kwa Liverpool na Sunderland na Tottenham Hotspur na Crystal Palace huku Queen Park Rangers waliwalaza vibonde wenzao Burnley 2-0.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Balotelli matatani tena

Liverpool nje Ulaya