in , , ,

MAHAKAMANI KUSIKILIZA KESI YA FEI TOTO WA YANGA

Fei Toto

HAKIMU; “Ndugu Feisal Salum Abdallah, maarufu kama Fei Toto, siku hizi wengine wanakuita Zanzibar

Feisal unashtakiwa na waajiri wako klabu ya Yanga katika mahakama hii kwa kosa la kuvunja mkataba

bila kufuata taratibu. Je unakubali kutenda kosa hilo? Na kama hukubali, je utakuwa tayari kuadhibiwa

kwa mujibu wa sheria na taratibu iwapo utapatikana na hatia?”

FEI TOTO; “Nashukuru sana mheshimiwa hakimu kwa kunipa nafasi kuwa mzungumzaji wa kwanza

katika shauri hili. Mheshimiwa hakimu nakiri mbele yako na mbele ya mahakama hii tukufu kwamba

nilivunja mkataba kwa kufuata utaratibu unaopaswa. Iwapo mahakama hii itagundua kwamba nilifanya

kosa au nilikiuka taratibu yoyote katika uvunjaji wa mkataba wangu na Yanga, nipo tayari kuadhibiwa

kwa mujibu wa sheria na taratibu.”

HAKIMU; “Ningependa utulivu uwepo wakati natoa nafasi kwa wakili namba moja upande wa utetezi

kuzungumza kwa niaba ya mshtakiwa. ikumbukwe karani wa korti yupo makini kurekodi kila tukio

linaloendelea kortini. Nizidi kusisitiza utulivu kutoka kwa wasikilizaji ili kumrahisishia kazi karani. Kama

upo tayari, ndugu wakili unaweza kuendelea.”

WAKILI NO 1; “Mheshimiwa hakimu nasimama kwa niaba ya mshitakiwa! Kama alivyokiri mteja wangu,

ni kweli kwamba ndugu Fey aliwasilisha barua ya kuvunja mkataba wake na Yanga katika tarehe tajwa

hapo awali. Kitu pekee tusichokubali ni kwamba, mteja wetu alifuata taratibu zote alizopaswa kufuata

katika mchakato wa kuvunja mkataba na waajiri wake wa zamani.”

“Mheshimiwa hakimu hii ni nakala ya mkataba walioingia Feisal Salum na Yanga miaka miwili iliyopita.

Katika mkataba huu, kipengele cha 14.7 kinatoa maelekezo jinsi ya mteja wetu kuvunja mkataba iwapo

ataona haja ya kufanya hivyo. Kipengele hicho kinaeleza kwamba, Feisal Salum atalazimika kulipa ada

ya usajili aliyoipokea wakati wa kusaini mkataba huu, pia atalazimika kulipa walau mshahara wa miezi

mitatu.”

“Mteja wetu alizingatia yote haya kama vilivoanisha vipengele vya mkataba ambao nimeuwasilisha

katika meza yako. Hivyo, mteja wangu hana kosa lolote na ninaomba mahakama hii tukufu ifutilie mbali

kesi hii.”

HAKIMU; “Wakili namba mbili upande wa mshitaki sasa ni nafasi yako”

WAKILI NO 2; “Mheshimiwa hakimu, ni kweli kipo na tunakitambua kipengele alichokizungumza ndugu

wakili. Lakini katika kipengele hicho, kimeelekeza vema kwamba mshitakiwa anaweza kuvunja mkataba

iwapo tu kutakuwa na hali isiyo ya kawaida.”

“Katika barua ya mshitakiwa hakueleza sababu ya kuvunja ya mkataba kama anavohitajika na kipendele

hiki. Aidha, mamlaka ya kusimamia soka duniani inaelekeza kwamba hali isiyo ya kawaida ni kama

kutokulipwa mshahara ndani ya miezi mitatu, kutocheza kwa muda mrefu na sababu zinazofanana.

Hivyo, mshitakiwa hakuwa na haki ya kuvunja ya mkataba huu. Ninaomba mahakama yako iamuru

Feisal Salum kuwa mali ya Yanga na sisi tutamchukulia hatua kulingana na sheria zetu.”

HAKIMU “Nitoe muda wa mapumziko wakati tukiendelea kujadili kabla ya kutoa hukumu. Tutaendelea

baada ya masaa mwili.”

(Wadau walipokutana nje muda wa mapumziko)

MDAU 1 ” Nimezungumza na Fey Toto, pale Yanga anaonewa sana. Hata mimi ningekuwa yeye,

ningeondoka. Fikiria kazi anayofanya na mshahara anaolipwa. Haviendani kabisa. Wale wageni

wanapewa pesa nyingi halafu hawafanyi kazi kubwa. Bora Fei Toto aondoke”

MDAU 2 “Tumia akili kidogo. Fei Toto hakulazimishwa kusaini mkataba na Yanga. wakati anasaini

alikuwa na akili timamu. Alikubali kulipwa mshahara anaolipwa kwa sasa. Kama analipwa mshahara

mdogo, angekataa kipindi ameitwa mezani kusaini mkataba”

MDAU 1 ” Fei Toto hataki kabisa kucheza Yanga. Bora wamuache aondoke kuliko kuwa na mchezaji

ambae hana mapenzi ya dhati na klabu”

MDAU 2 “Kwahiyo kila mchezaji akitaka kuondoka aseme sina mapenzi na hii klabu halafu aachiwe

huru? Kikubwa kama anataka kuondoka akae chini na Yanga wazungumze. Wakubaliane kiasi

anachopaswa kulipa kisha wamalizane. Au kama kuna timu inamtaka, wakae chini na Yanga

wamalizane”

MDAU 1 “Naona muda wa kusikia hukumu umefika. Twende ndani tukasikilize.”

HAKIMU “Baada ya kusikiliza pande zote mbili, mahakama hii imeamua kwamba mchezaji Feisal Salum

ni mali ya Yanga. Hivyo Feisal anapaswa kurejea Yanga na taratibu zingine zifuate. Aidha,nafasi ya rufaa

ipo wazi. Hivyo, mshitakiwa anaweza kukata rufaa katika mahakama ya juu zaidi.”

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0
Tanzania Sports

Kwa nini Arsenal wana nafasi ya kutwaa ubingwa England

cost Arsenal two points

Kuna aliyedhani VAR ingemaliza manung’uniko?