in , , , , ,

Mabosi wa Arsenal watikisa Dar

*watembelea Makao makuu ya PSPF
*wafanya mazungumzo na Mkurugenzi mkuu Bw Adam Mayingu

Mabosi wa Mabingwa wa Kombe la FA wa England, Arsenal, waliopo nchini kwa ziara ya kikazi wameanza kutikisa, ambapo kampuni nyingi zinataka ushirikiano na klabu hiyo.

Maofisa waliopo nchini ni pamoja na Mkurugenzi wa Maendeleo na Ushirikiano, Sam Stone na Meneja Maendeleo na Ushirikiano, Daniel Willey wanatarajiwa kukutana na uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Jumanne hii.

Tayari kampuni kubwa zaidi ya 20 zimetaka ushirika na Arsenal, na majadiliano ya kibiashara yanatarajiwa kuanza mara moja, kuona ni katika maeneo gani na kwa mfumo upi watashirikiana.

Katika ziara hiyo inayoratibiwa na Imani Kajula ambaye ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa EAG Group, benki mbalimbali zimetaka kufanya biashara na Arsenal, lakini pia Quality Group, kampuni inayomilikiwa na Rais wa Yanga, Yusuf Manji.

Stone amewaambia waandishi wa habari Jumatatu hii jijini Dar es Salaam kwamba wamejizatiti na japokuwa wamekuja kibiashara, milango ipo wazi iwapo kuna kampuni za michezo zinazotaka kushirikiana nao na kwamba zinaweza kunufaika.

Ujumbe huo umetua nchini huku hali ya hewa kisoka kwa klabu na timu ikiwa shwari, baada ya Arsenal kuwafunga Manchester City mabao 2-0 Jumapili hii kwenye Uwanja wa Etihad unaomilikiwa na mabingwa hao watetezi wa England.

Mabao ya Santi Cazorla na Olivier Giroud yakichanganywa na ulinzi mahiri wa kitimu, vilitosha kuzikonga nyoyo za washabiki wa Arsenal ndani na nje ya England, ambapo nchini Tanzania pia washabiki wao walionekana wakitamba mitaani, licha ya kwamba ilikuwa usiku.

Stone alisema jijini Dar Jumatatu kwamba wanaichukulia Tanzania kwa umuhimu mkubwa, kutokana na ukubwa wake kijiografia, mvuto wa watu wake kwenye soka na uwapo wa kampuni kubwa na zinazoweza kushirikiana na Arsenal.

Tayari Arsenal wana uhusiano na kampuni na taasisi nchini Kenya, Uganda, Rwanda, Afrika Kusini na Nigeria.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Maafisa wa Arsenal, waanza ziara yao Tanzania

AFCON 2015