in , , ,

Liverpool wawachapa Newcastle

Liverpool wawachapa Newcastle

Liverpool wamejirekebisha zaidi na kufika nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England baada ya kuwafunga Newcastle 2-0.

Raheem Sterling anayesuasua kusaini mkataba mpya alifunga bao la kwanza mapema dakika ya tisa na la pili likafungwa na Joe Allen.

Ufungaji huo umewafanya Liverpool kuwa na wafungaji 18 tofauti msimu huu.

Sterling aliyekataa kujadili mkataba mpya ambao angepata mshahara wa pauni 100,000 kwa wiki, ameingia kwenye tatizo jingine kwa kupigwa picha akivuta gesi aina ya nitrous oxide sebuleni mwake.

Tayari kocha wake, Brendan Rodgers amesema licha ya kwamba ni halali kisheria kuitumia, hadhani kwamba mwanasoka wa kulipwa anatakiwa kuivuta na kwamba atateta naye juu ya hilo.

Newcastle kwa kupoteza mchezo huo wameweka rekodi ya kufungwa mechi tano mfululizo, lakini Newcastle wataona wameonewa kwa kunyimwa penati ya wazi na pia mchezaji wao Moussa Sissoko alitolewa nje kwa kadi nyekundu kutokana na rafu mbili alizofanya dhidi ya Lucas Leiva ambaye, hata hivyo, hakuumia.

Liverpool wamefikisha pointi 57 nyuma ya Manchester City wenye 61, Manchester United 65, Arsenal 66 na Chelsea 73.

Southampton wanashika nafasi ya sita wakiwa na pointi 56, Tottenham Hotspur wakiwa was aba na pointi 54, Swansea wana 47, West Ham 43 na Stoke wanafunga 10 bora kwa pointi 43.

Mkiani wamebaki Leicester wenye pointi 25, Burnley 26 sawa na QPR.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Ubingwa unawaponyoka Man City

Kibarua cha Pellegrini hatarini