in , , ,

Liverpool waliwazidi Arsenal kwa Sanchez lakini …

Ilikuwa Barcelona wamuuze Alexis Sanchez kwa Liverpool kwa sababu walitoa kitita kizuri kuliko Arsenal, lakini raia huyo wa Chile alikataa kwenda Merseyside.

Liverpool walishatenga pauni milioni tatu zaidi ya Arsenal, hivyo wakawa na uhakika wa kumpata azibe pengo la Luis Suarez waliyemuuza Barcelona, lakini Sanchez akasisitiza kwamba anataka kuwa na Arsene Wenger.

Sanchez alisajiliwa majira ya kiangazi kutoka Barcelona kwa pauni milioni 32 hivi wakati Liverpool walikuwa tayari kutoa pauni milioni 35 au pungufu kidogo ya hapo.

Hata hivyo, Barca nao hawakuonekana kutoa shinikizo kwake, ikizingatiwa pia Arsenal walikuwa wamewauzia beki wa kati na nahodha wao, Thomas Vermaelen aliyekuwa anataka kwenda Manchester United. Arsenal pia waliwauzia viungo Alex Song na Cesc Fabregas miaka iliyopita.

Sanchez (25) ameshapachika mabao 10 katika mechi 15 alizopiga akiwa na Arsenal na aliondoka Barca kwa sababu hakuwa akipata muda wa kutosha wa kucheza. Amekuwa akicheza vyema na Danny Welbeck aliyesajiliwa kutoka Man United.

Tangu ahamie Arsenal, Sanchez ametokea kuwa kipendi cha washabiki wakati Liverpool walimpata Mario Balotelli ambaye ameshindwa kucheka na nyavu, akicheza namba tisa.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

JE, KUBADILI JEZI KUTASAIDIAJE MPIRA WETU TANZANIA?

Arsenal wajivuruga UCL