in , , ,

Lionel Messi ndani ya Afrika

*Aweka jiwe la msingi AFCON 2017 Gabon

Mchezaji bora wa dunia mara nne, Lionel Messi amewasili barani Afrika na kupewa heshima ya kuweka jiwe la msingi kwenye uwanja yatakapofanyika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2017 nchini Gabon.

Akiwa amevalia kaptula ya jinzi zinazopendwa na vijana, fulana nyeupe yenye picha aliungana na Rais wa Gabon, Ali Bongo Ondimba na maofisa wengine waliokuwa katika mavazi rasmi na kuweka jiwe hilo la msingi.

Messi aliwaongoza Barcelona kutwaa mataji matatu msimu uliopita – ubingwa wa Hispania, Kombe la Mfalme na Ubingwa wa Ulaya aliianzisha rasmi kazi ya ujenzi katika uwanja wa Port-Gentil utakaotumika kwa mechi hizo za 2017.

Hafla ya uzinduzi huo ilifanyika kwenye eneo kubwa lenye mchanga ambako uwanja husika utajengwa. Hii ilikuwa safari ya kwanza kwa Messi kufika nchini Gabon, ambapo pamoja na mambo mengine alitia saini yake kwenye vitu mbalimbali alivyoombwa, ikiwa ni pamoja na jezi za washabiki wake wanazovaa.

Rais Ondimba alitoboa siri kwamba alikutana na Messi jijini Barcelona miaka michache iliyopita na kumwambia kwamba angefika jijini Libreville kutembea na sasa anaona fahari kwamba mtu maarufu kama Messi ameitimiza ahadi hiyo, hivyo akamrejea kama mtu mwenye heshima.

Uwanja huo mpya utachukua washabiki 20,000 na unatarajiwa kutumiwa kwa ajili ya mechi mbalimbali kuanzia Novemba mwakani kuelekea kwenye michuano hiyo. Port Gentil ni jiji la pili kwa ukubwa nchini Gabon baada ya Libreville.

Michuano hiyo mikubwa zaidi barani itashirikisha timu 16 za mataifa mbalimbali, Gabon wakiwa tayari wamepitishwa kwa sababuya uenyeji. Tanzania walishatolewakatika hatua za awali.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Arsenal wachukua Barclays

KAGAME CUP YAZIDI KUPAMBA MOTO DAR