in , ,

Leicester mbele kwa mbele

 

Vinara wa Ligi Kuu ya England (EPL), Leicester wameendelea kuchanja

mbuga baada ya kupata ushindi mwembamba dhidi ya Norwich.

Ilikuwa mechi iliyodhaniwa kwamba ingemalizika kwa suluhu, lakini

vijana wa Claudio Ranieri walipata bao dakika ya 89.

Alikuwa ni Leonardo Ulloa aliyesababisha Leicester kuweka pengo la

pointi tano kileleni, baada ya kuunganisha majalo ya Marc Albrighton.

Pamoja na kwamba walicheza dhidi ya timu dhaifu na kutarajiwa

kuchomoza na ushindi mapema, Leicester ambao ni maarufu kwa jina la

Foxes hawakuwa kwenye kiwango chao cha juu na Norwich ndio

walitengeneza nafasi zaidi za kufunga.

Norwich waliwatega hivyo kwamba wenyeji walitegemea zaidi kupiga

mashuti kutoka mbali na waliendelea hivyo hadi Ulloa aliyetokea benchi

kupata fursa muhimu na kuitumia ipasavyo.

Laiti wasingefunga bao hilo, wangeweza kuondolewa kileleni Jumapili

hii ikiwa Arsenal au Tottenham Hotspur wangeshinda mechi zao, lakini

sasa wana uhakika wa kubaki kwenye kiti hadi mzunguko ujao, zikiwa

zimebaki mechi 12.

Msimamo wa EPL KWA Baadhi ya Timu
Msimamo wa EPL KWA Baadhi ya Timu

Norwich kwa kufungwa huko bado wapo nje ya eneo la kushuka daraja,

lakini wanafungana kwa pointi na waliomo humo, Newcastle, hivyo

watatakiwa kukaza mkanda kwenye mechi zilizobaki.

Katika mechi nyingine Jumamosi hii, West Ham waliwaadhibu Sunderland

kwa kuwapiga bao 1-0 na kuwaweka katka hatari kubwa ya kushuka daraja,

Southampton wakalala nyumbani kwao walipotandikwa 2-1 na Chelsea.

Stoke waliwazidi nguvu Aston Villa kwa 2-1, Watford wakatoshana nguvu

kwa 0-0 na Bournemouth wakati West Bromwich Albion waliwafunga Crystal

Palace 3-2.

Ligi hiyo inaendelea leo kwa Manchester United kuwakaribisha Arsenal

na Spurs watakuwa wenyeji wa Swansea.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

MAN U v ARSENAL JUMAPILI

Tanzania Sports

Arsenal wapotea njia