in ,

Kilio Arsenal, Spurs, Man City

 

*Manchester United wasogea taratibu

Vigogo wanaofukuzia ubingwa wa England nyuma ya Leicester wamepata

pigo kubwa, baada ya wote kufungwa na sasa wamebaki wakijiuguza

majeraha yao.

Leicester waliotangulia kucheza walibanwa kwa kwenda sare na West

Bromwich Albion Jumanne, kikawa kicheko kwa Arsenal, Manchester City

na zaidi sana Tottenham Hotspur ambao kama wangeshinda Jumatano hii

wangeongoza ligi.

Manchester United wao walikuwa na kicheko, kwani walifanikiwa

kuwafunga Watford 1-0, ukiwa ni ushindi wa nne mfululizo na

kumpunguzia shinikizo kocha Louis van Gaal. Bao la United lilifungwa

na Juan Mata katika dakika ya 83 kwa mpira wa adhabu ndogo.

Mshambuliaji chipukizi wa Man U, Marcus Rashford aliyetikisa katika

mechi mbili zilizopita kwa kufunga mabao mawili kila mchezo, usiku wa

Jumatano hii alikuwa kimya, lakini kwa upande wa Watford, Odion Ighalo

alipoteza nafasi mbili nzuri, na si ajabu kingekuwa kilio kwa timu nne

kubwa.

Rashford alibadilishana nafasi na chipukizi mwingine, Anthony Martial

kutoka Ufaransa, na ndiye alichezewa rafu na kusababisha mpira wa

adhabu uliotiwa kimiani na Mata kutoka umbali wa yadi 20.

Lakini kibao kikawageukia wababe hao watatu bila kuamini, ambapo Arsenal

walifungwa nyumbani na Swansea 2-1; Man City wakacharazwa 3-0 na

Liverpool huku Spurs nao wakipokea kisago cha 1-0 kutoka kwa West Ham.

Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kwamba tayari alikuwa na hofu

katika usiku huo ambao wababe watatu walikuwa uwanjani. Arsenal

wanabaki nafasi ya tatu, wakiwa pointi sita nyuma ya vinara Leicester

waliojikusanyia 57, ila Wenger anaahidi kwamba vijana wake watarudi

vyema.

Spurs wao walipoteza fursa ya kushika usukani wa ligi na sasa wamebaki

pointi tatu nyuma ya Leicester. Spurs wana mabao saba ya kufunga zaidi

ya vinara hao hivyo wangeshinda Jumatano hii wangeukamata uongozi wa

ligi.

Spurs watakutana na Arsenal Jumamosi hii, wakionekana kutojiamini na

wanaongezewa taabu kutokana na kuumia kwa mlinzi Laurent Koscielny na

golikipa Petr Cech.

Man City sasa wamebaki pointi 10 nyuma ya vinara lakini wana mechi

moja mkononi. Wanazo pointi 47 sawa na jirani na mahasimu wao

Manchester United. Mkiani mwa ligi wapo Aston Villa wenye pointi 16

wakipewa nafasi kubwa ya kushuka daraja, kwani wanaowafuatia juu ni

Newcastle, Norwich na Sunderland, wote wakiwa na pointi 24. Swansea

wanazo pointi 30 na kwa kuwafunga Arsenal wanaelekea kwamba

watajinasua kwenye kushuka.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

KESSY ANAWAPA SIMBA FUNZO WANALOSTAHILI

Tanzania Sports

JE UMEFIKA WAKATI WA ARSENE WENGER KUFUNGA VIRAGO?