in , ,

KAMATI YATANGAZA MCHAKATO WA UCHAGUZI TWFA

20120922-123736.jpg

Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) kimetangaza mchakato wa uchaguzi wa chama hicho ambao unaanza kesho (Septemba 23 mwaka huu).

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Ombeni Zavala, mchakato utaanza kesho ambapo fomu zitatolewa ofisi ya TWFA ambayo iko Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 10 jioni.

Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu ni Septemba 27 mwaka huu. Nafasi zinazogombewa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu, Mhazini, Mjumbe wa Mkutano wa TFF, na wajumbe watatu wa Kamati ya Utendaji.

Ada ya fomu kwa nafasi za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Katibu ni sh. 200,000 wakati nafasi zilizobaki ni sh. 100,000. Uchaguzi wa chama hicho kwa mujibu wa Kalenda ya Uchaguzi ya Wanachama wa TFF iliyotolewa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF utafanyika Novemba 4 mwaka huu.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 13 September 2012

Chelsea wagomea kileleni