in , ,

Kagame Cup, shwari….

Pamoja na awali kutandwa na hali ya

hofu ya usalama nchini Darfur ambako

ndipo yanafanyika michuano ya kombe la

Kagame mwaka huu hali ni shwari na

mashindano hayo yapo katika hatua ya

Fainali na tayari timu ya APR ya

Rwanda imekua ya kwanza kutinga hatua

ya fainali katika michuano hiyo.

Yanga ambao walikuwa mabingwa watetezi

wa michuano hiyo walivuliwa ubingwa

huo baada ya Serikali kuzikatazia timu

hizo za Tanzania Simba, Yanga na

Falcon ya Zanzibar kutokwenda katika

michuano hiyo kutoka na hali ya

usalama.

APR imekuwa ya kwanza kuingia katika

fainali baada ya kuifunga timu ya

wenyeji wa michuano hiyo Al Mereikh El

Fasher jumla ya magoli 4-3.

Ushindi wa APR unamfanya kocha wao

Andreas Spier kutimiza ndoto zake za

kuwania ubingwa huo katika fainali

zitakazofanyika Julai2 nchini humo.

Timu hizo zilimaliza muda wa kawaida

wa dakika 90 ikiwa sare ya 1-1 na

kutakiwa kuongezwa muda wa ziada wa

dakika30 ambapo APR ilimalizia karamu

ya magoli kwa kupachika magoli mengine

matatu.

Kwa ushindi huo sasa APR inasubiri

mshindi kati ya Vital O ya Burundi

dhidi ya Ryon Sports ya Rwanda katika

nusu fainali nyingine itakayopigwa leo

kwenye uwanja wa Nagwa mjini Durfur.

Kwa matokeo hayo yanaonyesha kuwa

fainali inachezwa na timu za ugenini

baada ya wenyeji wa michuano hiyo

kutolewa mapema katika michuamno hiyo

na kuwaachia wageni wakiendeleza ubabe

wa kutwaa kombe hilo kila mwaka.

Kwa upande wa Katibu mkuu wa Baraza la

vyama vya soka ukanda huu wa Afrika

Mashariki na kati CECAFA Nicholous

Musonye alisema licha ya klabu za

Tanzania kushindwa kushiriki lakini

michuano hiyo imefanyika vizuri na

imeonyesha msisimko mkubwa zaidi.

“Mashindano yamefanyika

vizuri,tunashukuru kila timu imevuna

ilichopanda,kutoshiriki kwa timu za

Tanzania hakujatuathiri chochote kwani

msisimko wa mashindano umeongezeka na

hata mashabiki wa nchini Sudan

wamefurahi kiwango cha timu

zilizoshiriki”alisema Musonye.

Hata hivyo Musonye alisema kuwa

hawatatoa adhabu yoyote kwa timu nza

Tanzania kushindwa kushiriki michuano

hiyo ila watawakaribisha tena mwakani

katika michuano mingine.

Michuano hiyo inataraji kufikia tamati

mapema Jumanne ijayo kwa mchezo wa

fainali.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Kwa nini Sunderland wawekeze Tanzania?

Arsenal wamchukua Yaya Sanogo