in , ,

HONGERA YANGA, UBINGWA UWE MAWANI YA KUONA PAKUBWA 

 

Lwandamina jana alifunga hesabu iliyofunguliwa na Hans Van Der Pluijm. 
Kitabu cha hesabu alichokabidhiwa na Hans Van Der Pluijm hakikuwa na 
hesabu nyepesi, akili kubwa ya ziada ilihitajika ili kufanikiwa 
kukokotoa hesabu hizi ngumu. 

Ndani ƴya miaka mitatu wamefanikiwa kuchukua ubingwa wa ligi kuu mara 
ya tatu mfululizo. Lakini katika misimu hiyo mitatu yote , msimu huu 
ndiyo ulikuwa msimu ambao ulikuwa na changamoto kubwa sana kwa Yanga. 

Ugumu mwingi wamepitia Yanga katika msimu huu ukilinganisha na misimu 
miwili iliyopita. Pamoja na kwamba msimi huu walianza vizuri kwa 
kufanikiwa kusajili baadhi ya wachezaji nyota kwa gharama kubwa kama 
Obrey Chirwa lakini mambo yalianza kubadilika lakini Yanga walitembea 
katika ugumu. 

Kwa wachezaji kuondokewa na kocha ambaye walikuwa wameshamzoea kuishi 
naye kwa muda mrefu tena akaondoka katikati ya msimu na kuletewa kocha 
mwingine mpya na wao kuonekana wanaweza kufanya kazi na mtu yoyote 
yule lilikuwa jambo ambalo lilionesha ukomavu kwa wachezaji wa timu ya 
Yanga. 

Ndani ya misimu mitatu iliyopita, ni msimu huu pekee ambao neno ukata 
limehubiriwa ndani ya kikosi cha Yanga. Kiuchumi Yanga haikuwa vizuri 
ukilinganisha na misimu miwili iliyopita. Hali hii ilisababisha 
wachezaji kutopata mishahara kwa wakati lakini wachezaji pamoja na 
benchi zima la ufundi lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa kutembea katika 
ugumu huu na kufanikiwa kuchukua ubingwa . 

Michuano ya kimataifa msimu huu , Ushiriki wa Yanga ulikuwa siyo mzuri 
kwani timu haikufanya vizuri ukilinganisha na msimu uliopita ambapo 
ilifanikiwa kufika hatua ya robo fainali ya kombe la shirikisho barani 
Afrika. Na hii ilisababishwa kwa kiasi kikubwa na hali mbaya ya uchumi 
iliyokuwa kwenye klabu ya Yanga. 

Msimu huu wamefanikiwa tena kupata ticket tena ya kushiriki michuano 
ya kimataifa baada ya kuchukua ubingwa. 

Ubingwa huu ambao wamechukua , wanatakiwa wasibweteke sana kwa kiasi 
kikubwa, kitu ambacho wanatakiwa wakifanye ni wao kukaa chini na 
kuanza kupanga mipango mizuri ambayo itawasaidia kufanya vizuri kwenye 
michuano ya kimataifa msimu ujao. 

Uzuri kuna neema imewashukia baada ya kupata udhamini wa Sport pesa 
hali itakayowasaidia kupunguza makali katika uendeshaji wa timu. 

Ni wakati sahihi kwao wao kukaa na benchi la ufundi vizuri na kuchukua 
tathimini ya kiufundi zaidi ili wajue ni aina gani ya wachezaji ambao 
watahitajika katika kikosi cha Yanga ili wafike mbali. 

Kipindi hiki Mascouts wa Yanga wanatakiwa kutumika vizuri kuwaleta 
wachezaji ambao ni hitaji la kocha na siyo hitaji la viongozi. 

Ule wakati wa kumsajili mchezaji fulani kutokana na matakwa ya 
kiongozi fulani bila kufuata ushauri wa kiufundi kutoka kwa kocha 
umeshapita. Ni wakati wa kufanya sajili za kiufundi na siyo za 
kisiasa. Ni vyema muda huu wakae na kujiuliza ni wapi walianguka msimu huu 
kwenye michuano ya kimataifa ili msimu ujao uwe kama msimu uliopita 
kwao. 

Wasiruhusu kubweteka na ubingwa huu hata kidogo, cha muhimu ni wao 
kutafakari kwa umakini ni kwa njia gani watakuwa imara kwenye michuano 
ijayo ya kimataifa. 

Report

Written by Martin

Martin Kiyumbi ni mchambuzi wa habari za michezo na mbunifu wa maudhui.

Martin Kiyumbi amewahi kufanya kazi za uchambuzi kwenye vituo mbalimbali vya habari kama Tanzaniasports (tovuti ya habari za michezo ), Jembe FM , Radio Free Africa na TVE.
Martin Kiyumbi anapatikana kwenye e-mail ya [email protected]

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

HIZI NDIZO SABABU ZILIZOIBEBA CHELSEA MSIMU HUU

Tanzania Sports

SportPesa Tanzania Welcomes Dar Giants Yanga SC To Its Family