in , , ,

Hatimaye, Suarez aomba radhi

*Ahaidi kutomng’ata mtu tena maishani!

Hatimaye mshambuliaji wa Uruguay, Luis Suarez ameomba radhi kwa kitendo chake cha kumng’ata Giorgio Chiellini wa Italia.

Mchezaji huyo wa Liverpool aliyefungiwa soka kwa miezi minne na mechi tisa za kimataifa amemtaka radhi Chiellini, akisema ni dhahiri aliumia.

“Ukweli ni kwamba jamaa yangu huyo Giorgio Chiellini aliumia mwilini kutokana na mng’ato ule tulipogongana naye. Najutia sana kwa hilo lililotokea.

“Naomba radhi kwa Giorgio Chiellini na ulimwengu wote wa wanasoka. Naahidi hadharani kwamba hapatatokea tena tukio jingine kama hili,” anasema Suarez.

Awali, Suarez (27) alidai kwamba alipoteza mizania, akayumba na wala hakumng’ata Chiellini. Hii ni mara ya tatu Suarez anatiwa hatiani kwa kung’ata wanasoka wa timu pinzani; mara ya kwanza ilikuwa Aprili mwaka jana akiwa Liverpool alimng’ata Branislav Ivanovic wa Chelsea na 2010 akiwa Ajax alimng’ata Otman Bakkal wa PSV.

Chiellini amemjibu Suarez kupitia mtandao wa Twitter akisema; “yameisha na nimeshasahau hayo. Natumaini Fifa watakupunguzia adhabu.”

Suarez atakosa mechi tisa za Ligi Kuu ya England na atarudi uwanjani Oktoba 26. Kutokana na ung’ataji wake kwa ujumla, atakuwa amekosa mechi 39.

Hata hivyo, taarifa yake ya kuomba radhi kwa tukio hili inafanana na aliyotoa mwaka jana alipomng’ata Ivanovic, ambapo licha ya kuomba radhi, alisema vitendo vyake havikubaliki uwanjani.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Kocha, nahodha Nigeria wajiuzulu

Kutoka TFF Leo