in , ,

Fifa mageuzi makubwa

 

Mkutano maalumu wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) umepitisha

mageuzi makubwa, yakilenga kurejesha hadhi yake baada ya kutikiswa na

umangimeza na ufisadi.

Pamoja na mambo mengine, kutakuwapo kuanikwa wazi mishahara pamoja na

ukomo wa muda wa urais wa Fifa. Baraza jipya la Fifa litachukua nafasi

ya kamati kuu ya sasa, na litatakiwa kuwa na walau mwanamke mmoja

kutoka kila shirikisho.

Baada ya kuidhinisha mabadiliko kadhaa, wajumbe wa mkutano mkuu huo wa

Fifa watafanya uchaguzi kupata rais mpya atakayechukua mikoba

inayoachwa na Sepp Blatter aliyekuwa katika nafasi hiyo tangu 1998.

Pamoja na kushinda kwenye uchaguzi wa mwaka jana, Blatter aliahidi

kuachia ngazi Ijumaa hii kwa sababu haoni akiungwa mkono na ulimwengu

wote wa soka. Alishauriwa tangu mwanzo asiwanie tena nafasi hiyo, na

kabla ya uchaguzi washirika wake kadhaa walidakwa na askari wa Uswisi

kwa maombi ya Marekani na wamefunguliwa kesi za utakatishaji fedha,

wizi na ubadhirifu wa mali ya umma.

Hata hivyo, alikuja kusimamishwa kazi na Kamati ya Nidhamu na Maadili

ya Fifa, baada ya kutiwa hatiani kujihusisha na mlungula yeye pamoja

na Rais wa Shirikisho la Soka la Ulaya (Uefa), Michel Platini

aliyekuwa anataka kugombea nafasi hiyo. Wote rufaa zao zimetupwa na

wanabaki na madoa.

Wagombea wanaowania urais wa Fifa ni Sheikh Salman bin Ebrahim

al-Khalifa, Gianni Infantino, Prince Ali bin al-Hussein, Tokyo Sexwale

na Jerome Champagne. Fifa imekuwan ikiongozwa na kaimu rais, Issa

Hayatou ambaye ni Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka la Afrika (CAF)

aliyesema kwamba Fifa itabaki kuwa moja na wanaoiunda watakuwa na

usharika mzito.

Viwango vya mishahara kwa rais wa Fifa, wajumbe wote wa baraza, katibu

mkuu na viongozi wa kamati maalumu na zile za kimahakama vitawekwa

wazi kila mwaka. Kuanzia anayechaguliwa leo, rais wa Fifa hatakaa

madarakani kwa zaidi ya vipindi vitatu vya miaka minne minne. Blatter

alikaa vipindi vitano.

Katika hatua nyingine, wajumbe wa mkutano huo wameamua kutenganisha

kazi za kisiasa na za kiutawala, ambapo baraza litawajibika kubuni

mkakati wa mwelekeo wa shirikisho hilo. Katibu mkuu wa Fifa atasimamia

utawala na masuala ya biashara katika utekelezaji wa mikakati husika.

Pamoja na viongozi mbalimbali wa soka wa sasa na wa zamani wa Fifa

kudakwa na askari na kushitakiwa, wadhamini mbalimbali wamekuwa

wakijiondoa ili kujitenga na uchafu wa Fifa. Mamlaka za Uswisi nazo

zinaendesha uchunguzi kwa maofisa wa Fifa.

Blatter anadaiwa kutoa hongo ya pauni milioni 1.3 kwa Platini ili

asimpinge kwenye uchaguzi wa 2011. Muda mfupi baada ya malipo hayo

Blatter alijitoa na kuwavuruda wadau waliokuwa wamepanga kumuunga

mkono ili kumng’oa Blatter.

Hata hivyo, wawili hao wanapinga kuwa ilikuwa hongo, bali wanadai

yalikuwa malipo halali kwa Platini aliyekuwa mshauri wa ufundi wa rais

wa Fifa (Blatter). Kinachoshangaza ni kwamba mshahara huo ulitolewa

miezi mingi baada ya kuwa amemaliza kazi hiyo na muda mfupi tu kabla

ya uchaguzi, kisha akajitoa kwenye kinyang’anyiro.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

Wenger: Barca wanapita

Tanzania Sports

MAN U v ARSENAL JUMAPILI