in , , ,

Man U hasara kubwa

Manchester United wanatarajia kupata hasara kubwa kifedha kutokana na kufanya vibaya kwa wachezaji wake uwanjani.
Klabu hiyo inatarajia kwamba mapato na faida zake katika mwaka ujao yataanguka kwa kiasi kikubwa, kutokana na, pamoja na mambo mengine, kushindwa kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya kwanza katika miaka 20.

Inaelezwa kwamba kipato halisi kimepungua kwa asilimia 84 kwa mwaka ulioishia Juni, ambapo walipata pauni milioni 23 ikilinganishwa na pauni milioni 146 mwaka mmoja tu uliopita wakati akiwapo Sie Alex Ferguson.

Kocha huyo mahiri alistaafu na nafasi yake kuchukuliwa na Mskochi mwenzake, David Moyes ambaye aliwatumbukiza Mashetani Wekundu kwenye moto usiozimika na kuishia nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi, wakati ndio walikuwa mabingwa watetezi.

Klabu hiyo ambayo kwa asilimia kubwa inamilikiwa na Familia ya Glazer wa Marekani, inasema kwamba katika mwaka wa fedha wa 2013/14 faida iliongezeka kwa asilimia 19 hadi kufikia pauni £433.2m kutokana na matangazo ya televisheni na udhamini.

Hata hivyo, sasa inatabiri kwamba gaida itashuka kwa kati ya £385m na £395m na faida inatarajiwa kushuka kwa kati ya £90m na £95m. Matokeo yanaonesha pia kwamba Moyes aliyefukuzwa kazi pamoja na benchi lake la ufundi walilipwa fidia ya pauni milioni 5.2 Aprili baada ya kuwa kazini kwa pungufu ya mwaka mmoja.

Hivi sasa United wanaye kocha mpya katika Louis van Gaal ambaye ameanza vibaya kwa kufungwa mechi ya kwanza ya ligi kuu, kwenda sare mechi nyingine mbili na kufungwa 4-0 na timu ya daraja la tatu ya MK Dons na kutupwa nje ya michuano ya Kombe la Ligi.

Hata hivyo, amefanya usajili wa wachezaji wengi wanaodhaniwa watasaidia kuirejesha klabu kwenye hadhi yake na kurudisha kuogopewa hasa wanapocheza kwenye uga wa nyumbani wa Old Trafford.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Mwanasoka afungiwa mechi 70

Oscar Pistorius hakuua kwa kukusudia