in , , ,

Fabregas: Nitarudi Arsenal

*Asema akitoka Barca ni Emirates tu

Nahodha wa zamani wa Arsenal, Cesc Fabregas anayekipiga Barcelona ya Hispania, amedokeza uwezekano wa kurudi Emirates.

Fabregas amesema kwa sasa anafurahia mambo yalivyo Nou Camp, lakini ikiwa ataondoka, chaguo lake la kwanza ni Arsenal.

Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger alisema mwezi uliopita kwamba anadhani ipo siku Fabregas atarudi kuchezea klabu hiyo ya kaskazini mwa London.

Kungo huyo aliwaacha Washika Bunduki wa London mwaka 2011 na kurudi kwenye klabu iliyomlea tangu akiwa mtoto ya Barcelona.

Alianza kucheza Ligi Kuu ya Uingereza mwaka 2003, lakini aliondoka Emirates kama ilivyo kwa nyota wengine, Thierry Henry, Patrick Vieira, Ashley Cole, Samir Nasri, Emmanuel Adebayor, Mathieu Flamini, Kolo Toure na Gael Clichy na kujiunga timu tofauti.

Mwezi uliopita pia, ripoti zilipindisha maneno ya Fabregas na kudaiwa alisema hatakaa arejee Arsenal, na sasa Mhispania huyo mwenye umri wa miaka 25 amesema yeye ni Arsenal damu.

“Sijazungumza na Wenger kuhusu hili, lakini ni habari njema kwangu, kwa sababu nilisikitika nilipoondoka.

“Nilipozungumza naye baadaye nilifurajia sana, kwa sababu niliweza kushikana mkono naye na kumwangalia machoni. Nisingejilaumu daima kama ningeondoka vibaya Arsenal, ni klabu kubwa, imenipa kila kitu.

English: Cesc Fabregas Warm-Up 30-01-2008, Emi...
English: Cesc Fabregas Warm-Up 30-01-2008, Emirates Stadium, London, UK. (Photo credit: Wikipedia)

“Nafarijika sana nikikumbuka mema mengi ya pale. Arsenal ndiyo chaguo langu siku zijazo kama nitaondoka Barcelona. Ndiyo timu ya kwanza ya chaguo langu, lakini kwa sasa hapa (Barcelona) sina tatizo,” anasema.

Barcelona walipokea kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa AC Milan kwenye michuano ya Kombe la Mabingwa Ulaya, na Fabregas alizungumza na waandishi kueleza kwamba watajitahidi kulipiza kisasi mechi ya marudiano.

Fabregas alianza kuchezea timu ya chipukizi Barcelona 1997 kabla ya kujiunga Arsenal 2003. Pia amechezea timu ya taifa ya Hispania ya vijana chini ya miaka 16 na ile ya wakubwa.

Enhanced by Zemanta

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Atletico watema ubingwa Europa

Manchester United hawakamatiki