in

EPL yazidi kupamba moto, huku Newcastle ikipoteza mchezo…

Mlinzi Ryan Taylor aliunawa mpira eneo la hatari na kusababisha Manchester City kupata bao lao la kwanza kwa mkwaju wa penalti uliojazwa kimiani na Mario Balotelli. Sergio Aguero baadae akatengeneza pasi murua kwa mlinzi Micah Richards aliyemaliza kazi kwa kufunga bao la pili.

Richards aliangushwa na Hatem Ben Arfa ndani ya eneo la hatari na kusababisha Manchester City wapate bao la tatu na penalti hiyo ilifungwa na Aguero.

Hata hivyo wakijitahidi dakika za mwisho Newcastle walifanikiwa kupata bao la kufutia machozi lililopachikwa na Dan Gosling baada ya kuuwahi mpira ambao ulipigwa na Demba Ba na kumgonga mlinda mlango Joe Hart.

Huo unakuwa mchezo wa kwanza kwa Newcastle kupoteza msimu huu.

Bao la dakika za mwisho lililofungwa na Leighton Baines kwa mkwaju wa penalti, liliipatia Everton ushindi wake wa pili wa ligi nyumbani msimu huu baada ya kuilaza Wolves mabao 2-1.

Stephen Hunt ndiye alikuwa wa kwanza kuipatia Wolves bao la kuongoza kwa mkwaju wa penalti baada ya kiungo Marouane Fellaini kumchezea rafu David Edwards ndani ya eneo la hatari.

Phil Jagielka aliisawazishia Everton baada ya kuunganisha kwa kichwa mpira wa free-kick uliochongwa na Baines kutokea upande wa kushoto.

Alikuwa Baines aliyeipatia bao la ushindi Everton zikiwa zimesalia dakika saba kabla mchezo kumalizika kwa mkwaju wa penalti baada ya Stephen Ward kumsukuma Louis Saha ndani ya sanduku.

Queens Park Rangers ikiwa imeanza kufungwa na Stoke, ilibadilika na kuweza kushinda kwa mabao 3-2 ambapo walisawazisha kwa bao la Heidar Helguson.

Stoke wakicheza uwanja wa nyumbani walipata bao la kuongoza lililowekwa wavuni na Jon Walters aliyeachia mkwaju mkali wa pembeni, kabla ya Helguson kusawazisha kwa kichwa akiwa hajakabwa na mchezaji yeyote.

Luke Young aliipatia QPR bao la pili kabla ya Helguson kuongeza la tatu kwa mkwaju wa karibu na lango.

Ryan Shawcross alifanikiwa kuipatia Stoke bao la pili naye kwa mkwaju wa karibu, lakini dakika nazo zilikuwa zimewatupa mkono na QPR ndio waliondoka na washindi.

Shane Long amerejea kwa kishindo katika klabu yake ya West Brom na kuinyanyua timu yake hadi nafasi ya 10 na kuzidi kuiongezea matatizo Bolton baada ya kufunga bao la pili la ushindi.

Mshambuliaji huyo alifunga bao lake la nne kwa msimu huu wa ligi katika dakika ya 56 ikiwa ni wiki nne tu tangu alipoumia goti.

West Brom ndio walikuwa wa kwanza kupata bao lililopachikwa na Jerome Thomas alipotegua mtego wa kuotea na akamzunguka mlinda mlango Jussi Jaaskelainen.

Ivan Klasnic alisawazisha dakika chache baadae kwa mkwaju wa penalti baada ya Fabrice Muamba kufanyiwa rafu, lakini hadi mwisho West Brom 2 Bolton 1.

Yakubu alikuwa shujaa wa Blackburn baada ya kufunga bao la kusawazisha kwa mkwaju wa penalti katika dakika ya 99 na kuipatia timu yake iliyokuwa ikicheza pungufu ya mchezaji mmoja sare ya mabao 3-3 dhidi ya Wigan.

Mshambuliaji huyo alisawazisha baada ya Wigan kuwa mbele kwa mabao 3-2.

Robin van Persie alikuwa mwiba wa kuotea mbali baada ya kuipatia timu yake ya Arsenal mabao 2-1 dhidi ya Norwich na timu hiyo kupata ushindi wake wa 10 kati ya mechi 12.

Van Persie akicheza kwa kiwango cha juu msimu huu, kwa mara nyingine alisaidia Arsenal kuweza kuamka na kuvuna pointi tatu ugenini.

Alipata bao lake la kwanza baada ya kuunganisha pasi ya pembeni kutoka kwa Theo Walcott na bao lake la pili lilitokana na pasi maridadi ya Alex Song.

Norwich walikuwa wa kwanza kuistua Arsenal walipofunga bao la kwanza lililofungwa na Steve Morison kutokana na makosa ya mlinzi wa Arsenal Per Mertesacker

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Premier League – Weekend previews

Van Persie fires Arsenal into last 16