in , , ,

EPL: upende usipende ndio hivyo

SIMULIZI za msimu wa soka wa Ligi Kuu England (EPL) 2018/19 zimeisha kwa habari zile zile za Liverpool kwamba wamekuwa wakifanya vyema lakini kombe hawapati.

Ni kama masuala ya upasuaji, ambapo madaktari nguli wanaweza kutoka kwenye chumba cha upasuaji na kuwaeleza mwenye mgonjwa wao kwamba upasuaji ulikuwa wa mafanikio makubwa lakini mgonjwa alifariki dunia.

Maana ya hiyo ni kwamba taratibu zote za kumwandaa mgonjwa, ukusanyaji vifaa pamoja na zoezi zima la upasuaji vilienda kwa mujibu wa taratibu na maadili ya utabibu, mbaya tu ni kwamba mgonjwa alipoteza maisha yake.

Manchester City wametetea ubingwa wao kwa mara ya pili, ukiwa ni msimu wa tatu kwa kocha Pep Guardiola kuwa nao Etihad Stadium, na huyu ndiye Guardiola tunayemjua, tangu Baracelona hadi Bayern Munich.

Liver walisumbua sana lakini wameshindwa kwa alama moja tu, wakifunga jamvi wakiwa na alama 97, kama kawaida Jurgen Klopp akionesha kutosikitika kivile, japo alikuwa na hamu nay eye anyanye kombe.

Pilika Pilika za EPL 2018/19

Wapo wanaosema kwamba Klopp ni mmoja wa makocha wasiokuwa na bahati zaidi katika EPL kwa soka ya nyakati hizi, kwa jinsi makombe yanavyomponyoka huku akiwa na kikosi kipana.

Chelsea waliosuasua hatimaye walijiimarisha katika dakika za mwisho chini ya Maurizio Sarri, na kufanikiwa kufuzu kwa michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL) sambamba na Tottenham Hotspur.

Hiyo pia ilitokana na kuzorota kwa Arsenal waliofungwa mechi hovyo kuelekea mwisho wa ligi hiyo, wakati Manchester United kama walivyotarajiwa, wamekuwa nje ya nne bora na kwao na Ligi ya Europa mwakani.

Wakati hali ikiwa hivyo huko juu na wengine hapo katikati wakiwa kimya, kule chini wameshuka daraja akina Huddersfiend, Fulham na Cardiff.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

UCL na Europa: Wanaofuzu kwa msimu ujao

Tanzania Sports

EPL: Mabadiliko msimu mpya uwanjani