in , , ,

Drogba kurudi Chelsea? Ni tetesi za usajili..

*Dili la Costa bichi, Man U nao wamo
*Arsenal wakamilisha usajili wa kwanza

HARAKATI za kusaka wachezaji kwa usajili wa majira ya joto zimeanza lakini mchakato unaelekea kuwa mrefu.
Hata Diego Costa wa Atletico Madrid aliyedaiwa kwamba ameshasainiwa na Chelsea bado hajajua hatima yake, kwani klabu yake kwanza ilidai haikuwa na habari za yeye kwenda Chelsea.

Jumamosi hii wakuu wa Chelsea walieleza kusikitishwa kwao na mchakato wa usajili wake kusuasua, ambapo licha ya kupimwa afya yake Stamford Bridge na kurudi kwenye timu ya taifa, Atletico wamekaa kimya kana kwamba hakuna lolote walilojulishwa.

Chelsea wametimiza masharti ya kifungu cha mkataba wake, kwamba Costa (25) anaweza kusajiliwa kwa dau la pauni milioni 32 na kwamba mchezaji huyo ameshawajulisha Atletico juu ya Chelsea kumtaka na yeye kuridhia lakini wamekaa kimya. Arsenal walifikia matakwa ya kifungu cha kumsajili Luis Suarez msimu uliopita lakini Liverpool wakakataa kumtoa.
 
DROGBA KURUDI CHELSEA?

Tetesi zilizopo ni kwamba Chelsea wanataka kumsajili mpachika mabao wao wa zamani, Didier Drogba anayemaliza mkataba wake Galatasaray.
Kocha Jose Mourinho anaangalia uwezekano wa kumsajili Drogba (36) aliyewasaidia Chelsea kutwaa ubingwa wa Ulaya kabla ya kuondoka. Chelsea pia wanataka kumsajili mlinzi wa Atletico, Miranda.
 
MAN U WAMTAKA POGBA

Manchester United wanataka kumrejesha mchezaji wake wa zamani, Paul Pogba anayekipiga Juventus na ambaye hakupewa nafasi ya kung’ara chini ya Alex Ferguson.
Hata hivyo, Juventus wanadaiwa kutotaka kuuza mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umriw a miaka 21.
Kocha Louis van Gaal wa United anataka kuvamia Ujerumani na kusajili wachezaji watatu; Mats Hummels, Bastian Schweinsteiger naThomas Mueller.
 
ARSENAL NA USAJILI WA KWANZA, BALOTELLI

Wakati Arsenal wamekamilisha usajili wa mchezaji wao wa kwanza kwa msimu ujao, wanadaiwa sasa kuendelea na mchakato wa kuwapata Mario Balotelli wa AC Milan na Loic Remy wa Queen Park Rangers (QPR).

Inaelezwa kwamba AC Milan wanataka kuondokana na Balotelli, japokuwa anauzwa kwa dau kubwa la pauni milioni30 ili wanunue mchezaji mwingine mwenye nidhamu, na Arsenal wanaonekana ndio wenye kumhitaji katika kuboresha safu yao ya ushambuliaji.

Arsenal wamekamilisha usajili wa kinda la Kigiriki, Elias Chatzitheodoridis (17) baada ya kuwafurahisha makipa. Alikuwa akichezea klabu ya Mas Kallitheakos lakini pia alikuwa akifanya mazoezi na academia ya Arsenal iliyopo Ugiriki.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Oxlade-Chaberlain fiti Kombe la Dunia

Azim awapasha TFF