in , , ,

Chelsea watandikwa 3-0

*Fabregas alambwa kadi nyekundu

West Bromwich Albion wametibua mwendelezo wa sherehe za ubingwa wa Chelsea kwa kuwatandika mabao 3-0.

Katika hali ya kushangaza, kocha Jose Mourinho amelalamikia klabu nyingine kwa kichapo hicho, akidai hazikuonesha ushindani wa kutosha kwenye Ligi Kuu.

Aliyeanza kupeleka kilio kwa The Blues alikuwa ni mzaliwa wa Burundi, Saido Berahino ambaye pia alifunga la pili kwa penati kabla ya Chris Brunt kutia la tatu.

Penati hiyo ilitolewa baada ya nahodha wa Chelsea, John Terry kumwangusha Beraniho ndani ya eneo la penati.

Chelsea walimaliza mechi wakiwa 10 baada ya kiungo wake wa kimataifa wa Hispania, Cesc Fabregas kupewa kadi nyekundu.

Fabregas alipewa kadi nyekundu kwa kitendo chake cha kumpiga kwa mpira Brunt. Hiki kilikuwa kipigo cha tatu kwa Chelsea kwenye ligi msimu huu.

Kabla ya mechi hii Chelsea walikuwa wamekwenda michezo 16 bila kufungwa. Mshambuliaji wa kati wa Chelsea, Diego Costa naye alionekana kukwaruzana na beki wa kati wa West Brom, Gareth McAuley kiasi cha mwamuzi Mike Jones kuingilia kati kuwapatanisha.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Yanga, Simba mbio za usajili

Sterling hawataki Liverpool