in , , ,

Chelsea wapigwa, kocha ajifariji

 

Kocha wa mpito wa Chelsea, Guus Hiddink anaamini timu yake watavuka

hadi robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL) licha ya kufungwa na

Paris Saint-Germain 2-1.

Hiddink anasema kwamba bado wana fursa ‘50-50’ ya kusonga mbele,

ikizingatiwa kwamba walifungiwa ugenini na wao kupata bao moja, kwenye

mechi hiyo ya mkondo wa kwanza katika hatua ya 16 bora.

Alikuwa ni Zlatan Ibrahimovic aliyeanza kucheka na nyavu za Chelsea

kabla ya John Mikel Obi kusawazisha, lakini Edinson Cavani akawapa

wenyeji ushindi.

Mechi ya marudiano itafanyika Stamford Bridge Machi 9 na Hiddink

anasema alifurahi kwamba walifunga, japokuwa alisikitika kupoteza

mechi.

Huu ni msimu wa tatu mfululizo Chelsea wanakutana na PSG katika mechi

hizo, ambapo msimu uliopita mabingwa hao wa England walitolewa katika

hatua kama hii na PSG.

Cavani, mshambuliaji wa Uruguay aliyejiunga PSG kwa pauni milioni 55

mwaka 2013, alitokea benchi na kuwapa bao muhimu mabingwa hao wa

Ufaransa.

Chelsea wka upande mwingine kwenye benchi lao walikuwa na akina Ruben

Loftus-Cheek, Bertrand Traore, Kenedy na Matt Miazga, ndipo Hiddink

akasema aliwaonea wivu PSG kuweza kumweka benchi mtu kama Cavani.

“Niliwaonea wivu kidogo jinsi walivyokuwa na kikosi kizito uwanjani na

benchi pia. Ukiona kile timu ilicholeta kipindi cha pili – ni

wachezaji wa kimataifa hasa waliokuwa benchi. PSG ni timu kubwa sana,”

akasema Mdachi huyo.

Cavani kwa muda mwingi amekuwa akitumiwa kama papili wa Ibrahimovic au

akicheza nyuma yake, yaani namba 10.

Kwa hali hiyo amekuwa akihusishwa na kutaka kuhamia timu nyingine ili

apate muda zaidi wa kucheza, hasa kama mshambuliaji wa kati, nafasi

anayoimudu vyema.

Katika mechi nyingine ya UCL, Benfica waliwafunga Zenit St-Petersburg

1-0, kwa bao la dakika za majeruhi la kichwa la Jonas, wakicheza

nyumbani.

Mshambuliaji huyo wa Brazil aliutendea haki mpira wa adhabu ndogo wa

Nicolas Gaitan, na ni bao lake la 25 msimu huu.

Mlinzi wa wageni, Domenico Criscito alitolewa nje baada ya kupata kadi

mbili za njano kwa kucheza rafu.

Benfica walicheza vyema zaidi katika kipindi cha pili dhidi ya Zenit

ambao hawakuwa wamecheza mechi kwa wiki 10 hadi hii ya Jumanne, kwani

ligi ya kwao ipo katika mapumziko ya msimu wa baridi.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

Utata penati ya Messi

Tanzania Sports

YANGA YAUA MNYAMA, YAREJEA KILELENI.