in , , , ,

Chelsea wamtwaa Mohamed Salah

Klabu ya Chelsea imemsajili winga wa Basel ya Uswisi kutoka Misri, Mohamed Salah aliyewatesa kwenye mechi za Ligi ya Europa.

Usajili huo unadaiwa kuwa na gharama ya kadiri ya pauni milioni 11 na unakuja wakati klabu hiyo imemwachia kiungo mchezeshaji Juan Mata kwenda Manchester United kwa pauni milioni 37 hivi ambazo si kawaida Man U kuziachia kihivyo.

Salah (21) alitarajiwa kuchukuliwa vipimo kiafya hapo Stamford Bridge na pia kukutana naye kwa ajili ya makubaliano baina yao na yeye kwa mafao yake.

Hatua hii inakuja wakati Liverpool walishaanza mazungumzo na Basel kwa ajili ya kumchukua raia huyo wa Misri kwa ajili ya kumsajili kwenye dirisha dogo Januari hii.

Chelsea tayari wamemsajili Nemanja Matic. Salah aliwafunga Chelsea kwenye nusu fainali ya Europa mwaka jana kabla ya kupata bao pekee dhidi ya klabu hiyo ya kocha Jose Mourinho Desemba katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Man United wapigwa tena Old Trafford