in , , ,

Chelsea wamtaka kocha Conte

 

*Van Gaal akomaa haondoki Man United

*Cahil hofu Chelsea, Big Sam majina 60

Tetesi za nani atachukua nafasi ya Jose Mourinho klabuni Chelsea

zinazidi kutanuka.

Mpya mjini sasa ni kwamba wanamtaka kocha wa Timu ya Taifa ya Italia,

Antonio Conte, 46, anaweza kuchukua kiujumla mikoba ya The Special

One.

Baada ya kufukuzwa kazi kwa Mreno huyo, nafasi yake inashikiliwa kwa

muda, na kwa mafanikio kiasi, na Guus Hiddink aliyepata pia kuingia

Stamford Bridge kuwaokoa walipotaka kuzama.

Mtaalamu huyo anatarajiwa kuondoka mwishoni mwa msimu huku mmiliki

Roman Abramovich na viongozi wa Chelsea wakiumiza vichwa kupata bosi

wa kudumu.

Zimekuwapo tetesi pia kwamba Chelsea wanamfikiria kocha wa Tottenham

Hotspir, Maricio Pochettino anayefanya vyema White Hart Lane.

Lakini pia, zipo habari kuwa wanamfikiria kocha wa Bournemouth, Eddie Howe.

Hata hivyo, mwekezaji wa Bournemouth kutoka Marekani, Matt Hulsizer

anasema kwamba Howe, 38, haendi popote, akimaanisha hatamwachia.

Baadhi ya wadau wakidai Pep Guardiola ndiye chaguo tayari, japo

Manchester City wandaiwa wanamtaka akavae viatu vya Manuel Pellegrini

anayekosa uendelevu.

Hatima ya kocha wa Manchester United, Louis van Gaal inaendelea

kupamba vichwa vya magazeti mengi ya hapa, baadhi yakidai kwamba yupo

njiani kuondoka.

Hata hivyo, yeye mwenyewe anasema kwamba yupo Old Trafford na haendi

popote, ndiyo maana amekuwa akitafuta nyumba nyingine.

Anataka kuhakikisha anamaliza mkataba wake wa miaka mitatu aliosaini

hapo, na wakala wake alikuwa akimtafutia nyumba eneo la Cheshire.

Akizungumza kabla ya mechi ya Ijumaa hii dhidi ya Derby, Van Gaal

amesema kwamba akishindwa mechi hiyo anaweza ‘kufukuzwa kwa mara ya

nne’, akionesha kuwabeza waliosema kwamba amefikia kufukuzwa kazi mara

tatu.

Zimekuwapo habari pia kwamba Guardiola kuaga kwake Bayern Munich

mwishoni mwa msimu kunamaanisha anaingia United.

Pia Mourinho ameshatuma barua United akiomba apewe nafasi ya Mdachi

huyo anayedaiwa kushindwa kufikia mafanikio tarajiwa.

Kadhalika tetesi nyingine ni kwamba Makamu Mwenyekiti Mtendaji wa Man

U, Ed Woodward na viongozi wenzake, wana wasiwasi katika kufanya

uamuzi hata akiondoka Van Gaal, kwani wasipompa nafasi hiyo kocha

msaidizi Ryan Giggs, na kwamba anaweza kukatisha miaka yake 18

aliyokaa Old Trafford kama mchezaji, kocha wa mpito na sasa kocha

msaidizi.

Manchester United wanamtaka mshambuliaji wa CSKA Moscow kutoka

Nigeria, Ahmed Musa, ambaye tayari anawaniwa na vinara wa Ligi Kuu ya

England, Leicester.

Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp anafikiria kutoa pauni milioni 11 kwa

ajili ya kumnunua kiungo wa Udinese na raia wa Poland, Piotr

Zielinski, 21.

Mlinzi wa Chelsea, Gary Cahill, anayehofia kuikosa michuano ya Euro

2016, anatakiwa na klabu ya Italia ya Roma. Cahil ametupwa benchi na

kocha Hiddink kwa muda sasa.

Mchezaji huyo wa zamani wa Aston Villa na Bolton mwenye umri wa miaka

30 angewafaa Liverpool kuboresha ngome yao.

Mshambuliaji wa Barcelona, Neymar, 23, anasema angependa kucheza chini

ya kocha Pep Guardiola, hivyo kuacha maswali iwapo atasubiri aone

anakwenda wapi ndipo wakala wake aunganishe mambo.

West Bromwich Albion wanafanya mazungumzo na Queens Park Rangers (QPR)

kwa ajili ya kumpata kwa mkopo mchezaji wa zamani wa Spurs, Sandro.

Mlinzi wa New York Red Bulls, Matt Miazga, 20, alikuwa London Alhamisi

hii kwa ajili ya vipimo vya afya kabla ya kujiunga Chelsea.

Arsenal wamekataliwa ofa yao ya pili waliyopeleka Leicester kwa ajili

ya mlinzi wao mwenye umri wa miaka 19, Ben Chilwell.

Newcastle wanafikiria kuachana na mipango ya kumsajili mshambuliaji wa

West Brom, Saido Berahino na kutafuta mchezaji mbadala.

Magpies walikuwa tayari kutoa pauni zaidi ya milioni 20 kumpata

mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 lakini West Brom hawatoi

ushirikiano.

Newcastle wanatarajiwa kumfuata mshambuliaji wa Chelsea, Loic Remy,

29, aliyefunga mabao 14 katika mechi 26 za ligi kuu alipokuwa

Newcastle kwa mkopo msimu wa 2013/14.

West Ham na Norwich wanapigana vikumbo kumsajili mlinzi wa Inter

Milan, Davide Santon, 25.

Manchester United wanataka kumsajili kiungo Mreno wa Chelsea, Domingos

Quina, 16, aliyeingia akademia ya Stamford Bridge akiwa na umri wa

miaka 13.

Kocha wa Sunderland, Sam Allardyce amesema ana orodha ya majina ya

wachezaji 60, na kutoka humo atapata wa kusajili katika dirisha hili

dogo linalofungwa mapema Februari.

Katika hali ya kushangaza, kocha wa Crystal Palace, Alan Pardew tayari

ana wasiwasi kwamba mchezaji wake mpya, Emmanuel Adebayor, 31, anaweza

kuondoka bure mwishoni mwa msimu.

Adebayor amekuwa mtovu wa tabia lakini pia ameonekana kuathirika

kisaikolojia baada ya kukorofishana na familia yake – mama mzazi, kaka

na adada yake, akidai wamekuwa wakimloga ili ashuke kiwango alipokuwa

Spurs.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

Arsenal wanyonge kwa Chelsea

Tanzania Sports

PSPF yatoa msaada wa viti