in ,

Chelsea nje Kombe la FA

 

*Man City wavutwa shati EPL

Chelsea wameendelea kupata mapigo, baada ya kutupwa nje ya michuano ya

Kombe la FA na Everton.

Alikuwa Romelu Lukaku, mchezaji wao wa zamani ambaye hakupendwa na

bosi aliyefukuzwa kazi, Jose Mourinho aliyewapa maangamizi.

Katika mchezo huo, mshambuliaji wa Chelsea ambaye amehusishwa na

matukio kadhaa ya utovu wa nidhamu, Diego Costa, anadhaniwa kumng’ata

mchezaji wa Everton, Gareth Barry na wote kuishia kupewa kadi

nyekundu, lakini kwa matukio tofauti.

Makocha wao, Guus Hiddink na Roberto Martinez hawakutoa kauli ya

kumshutumu yeyote. Mabao ya Everton yalifungwa na Lukaku na Barry

Pengine Chelsea watajilaumu kwa kumwacha Lukaku aondoke, ambapo akiwa

na umri wa miaka 22 tu ameshafunga mabao 25 katika mashindano yote

msimu huu.

Katika Ligi Kuu ya England, Manchester City walibanwa na Norwich kwa

kwenda suluhu wakati Bournemouth wakiwapiga Swansea 3-2 na Stoke

wakiwa nyumbani wakilala kwa 1-0 dhidi ya Southampton.

Hali hiyo inawaacha vinara Leicester kuwa juu kwa pointi 60, Tottenham

Hotspur wa pili kwa pointi 55, Arsenal wa tatu na zao 52 wakati Man

City wanazo 51.

Mkiani wamo Aston Villa na pointi 16 wakiwa chini ya Newcaste wenye

pointi 24 na Norwich wenye pointi 25.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

YANGA YAWANYOOSHA APR JIJINI KIGALI

Tanzania Sports

Leicester wazidi kupaa