in , , ,

Brazil watawamudu Wajerumani?

Hatua za nusu fainali za michuano ya Kombe la Dunia huacha historia isiyofutika katika ulimwengu wa soka.
Wakati mwingine ile ari, nguvu na kasi inayotumika kutaka kufika hatua ya mwisho hutoa ushindani ambao wakati mwingine huzidi hata fainali yenyewe.

Ni timu nne zinazotaka kujihakikishia zinafika fainali ili kumtwaa mwali, na kwa kuanzia Jumanne hii itawashuhudia wenyeji Brazil waliojeruhiwa wakishuka dimbani kuchuana na Ujerumani.

Vijana wa Luiz Felipe Scolari wanashuka dimbani wakiwa hawana nyota wao wa ushambuliaji, Neymar aliyeumizwa uti wa mgongo katika emchi ya robo fainali dhidi ya Colombia na pia hawatakuwa na nahodha wao, Thiago Silva ambaye anatumikia adhabu ya kupata kadi mbili za njano.

Kocha Scolari anajipa moyo na kuwatuliza washabiki wao, akisema kwamba wanaweza kucheza vyema hata bila ya kuwapo Neymar uwanjani, huku Silva akiwataka wenzake wahakikishe wanashinda ili iwe zawadi kwa Neymar (22).

Kinda huyo ndiye amefunga mabao manne kati ya manane waliyo nayo Brazil hadi sasa lakini Scolari anasema kikosi chake kina ari kubwa, kikiwa tayari kuwavaa Wajerumani. Mshambuliaji wao mzuri, Fred, alionekana kutokuwa vyema sana kwenye mechi zilizopita.

“Neymar ameshatoa mchango wake, sasa ni juu yetu kutoa wa kwetu. Tumeshapokea yaliyotokea na sasa tunajielekeza kwenye mambo mengine,” anasema Scolari akiwa hataki kuzama kwenye suala moja la kumkosa Neymar tofauti na wanahabari wanavyopenda.

Neymar alitenguliwa pingili ya uti wa mgongo na mchezaji wa Colombia, Juan Zuniga aliyemgonga kwa goti kutoka nyuma na kumpa maumivu makali kiasi cha kulia machozi kwa sauti kubwa uwanjani hadi akiwa hospitalini.

Kocha wa Ujerumani, Joachim Low alisema kwamba anadhani Wabrazili ni wazuri bado na kwamba wanaweza kuwasababishia majanga, ila akamhadharisha mwamuzi wa mechi hii, Marco Antonio Rodriguez kuwa makini na kuchukua hatua dhidi ya kila rafu lakini pasipo kuonea wala kupendelea upande wowote.

Mjerumani huyo anasema kwamba mechi baina ya Brazil na Colombia ilihusisha kutunishiana misuli na rafu nyingi sana na si dhidi ya Neymar pekee, akisema kwamba hajapata kuona soka ya aina hiyo Ulaya, akamtaka mwamuzi awalinde wachezaji muda wote wa mchezo.

Mechi hii inapigwa katika dimba la Estadio Mineirao, jijini Belo Horizonte, uwanja unaokalisha watazamaji zaidi ya 62,000, ambapo watu waliowasili kwenye uwanja wa ndege jijini humo Jumatatu hii walipokewa kwa bendera na mabango ya Brazil, wakiwa na hamu ya kununua tiketi kwa ajili ya mechi hii kubwa.

Brazil wamekutana na Ujerumani katika Kombe la Dunia mara moja tu, mwaka 2002 katika fainali nchini Japan, ambapo Scolari aliwaongoza vijana wakashinda 2-0 na kutwaa kombe hilo.

Ujerumani wanacheza nusu fainali ya nne mfululizo katika mashindano haya tangu wakati huo, Low akisema vijana wake watakuwa kana kwamba wanakabiliana na nchi nzima ya Brazil, kwani watakuwa wanaungwa mkono na watu milioni 200.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Di Stefano shujaa wa soka afariki

ALIANZA ALPHONSUS DIKE KABLA YA LOUIS VAN GAAL