in , , ,

Bournemouth, Watford kamili EPL

 

*Ubingwa wa EPL waenda Bournemouth

 

Bournemouth waliofanikiwa kutinga Ligi Kuu ya England (EPL) msimu ujao wametwaa ubingwa katika Ligi Daraja la Pili maarufu kama Championships.

 

Bournemouth walicheza vyema Jumamosi hii katika siku ya mwisho ya ligi hiyo, wakipata ushindi mnono wa 3-0 dhidi ya Charlton.

 

Waliokuwa wakipewa nafasi ya ubingwa, Watfrord, waliteleza dhidi ya Sheffield Wednesday kwa kwenda sare.

 

Mabao ya Bournemouth ayalifungwa na Matt Ritchie aliyetia mawili na Harry Arter kuhakikisha ushindi kwa vijana hao wa kocha Eddie Howe.

 

Bournemouth sasa wamemaliza ligi wakiwa na pointi moja mbele ya Watford na timu zote hizo mbili zimepanda daraja na zitaonekana EPL msimu ujao.

 

Mwisho wa ligi hiyo unatoa nafasi kwa mechi za mchujo tena kupata wa kuungana na timu mbili zilizopita. Timu zitakazocheza mtoano ni Norwich, Middlesbrough, Brentford na Ipswich.

 

Timu zilizoshuka kutoka daraja hilo kwenda chini zaidi ni pamoja na zilizopata kucheza EPL, Wigan na Blackpool pamoja na Milwall.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

TETESI ZA USAJILI

Mayweather ampopoa Pacquiao