in , , ,

Balotelli matatani tena

“KWA nini mimi kila wakati?” ni swali ambalo mshambuliaji aliyetokea kuwa butu wa Liverpool, Mario Balotelli amekuwa akijiuliza hadi kuliandika kwenye fulana yake anayovaa ndani ya jezi.

Safari hii ameingia tena matatani, kwani Chama cha Soka (FA) kimemshitaki kwa makosa ya kupandisha katika mtandao wa jamii maneno yanayoonekana kuwa ya kibaguzi.

Balotelli (24) aliweka kwenye mtandao wa Instagram picha ya mhusika wa kwenye michezo ya kompyuta, Super Mario, iliyokuwa na maneno ya Kiingereza yanayomaanisha ‘anaruka kama mtu mweusi na kupokonya sarafu kama Myahudi’.

Hata hivyo, mchezaji huyo wa Timu ya Taifa ya Italia, baada ya kufanya hivyo alituma ujumbe kupitia mtandao wa Twitter akikanusha kuwa na nia mbaya kwa maneno hayo, na baada ya hapo aliomba radhi.

FA wamempa hadi saa 12 jioni ya Desemba 15 awe amejitetea, ambapo msemaji wa Liverpool amekiri juu ya uamuzi wa FA na kwamba mchezaji huyo atafuata hatua takikana kujibu mashitaka yake.

Balotelli anadai kwamba alitumia kikaragosi kilichotengenezwa na mtu mwingine, akidhani kwamba ilikuwa katika kutaniana tu, akisema si kweli kwamba weusi wote wanaweza kuruka juu sana wala kwamba Wayahudi wote wanapenda sana pesa.

Liverpool ana majeraha na amekosa mechi kadhaa, kama itakavyokuwa Jumamosi hii kwenye mechi dhidi ya Sunderland. Amefunga mabao mawili tu katika mechi zake 14 msimu huu kwa Liverpool.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Chelsea waoga kichapo cha kwanza

Majanga Arsenal