in , ,

Atletico mabingwa Hispania

 

Atletico Madrid wamefuta uteja kwa klabu mbili kubwa za Real Madrid na Barcelona kwa kutwaa ubingwa wa nchi.

Atletico wanaofundishwa na Diego Simeone walitwaa ubingwa kwa staili ya aina yake, kwani waliwavua mabingwa watetezi, Barcelona.
Zaidi ya hapo, waliwatoa nishai kwa kuwalazimisha sare ya 1-1 kwenye mechi ya mwisho ya msimu na kuipata pointi moja tu waliyokuwa wakihitaji.

Barca walikuwa wanahitaji pointi tatu ili kutetea ubingwa wao lakini licha ya kuwa na wachezaji maarufu duniani hawakufurukuta.
Kutokana na hali hiyo, Kocha wa Barcelona, Gerardo Martino ‘Tata’ ameamua kuachia ngazi na kuwaomba radhi washabiki kwa kushindwa kutimiza ndoto yao.

Tata alichukua nafasi hiyo kwa mkataba wa miaka miwili lakini ameondoka kabla hata ya kufikia nusu, akiwa amerithi nafasi ya hayati Tito Vilanova aliyejiuzulu kwa sababu ya maradhi ya saratani ya shingo.

Atletico wamefikisha pointi 90 na kuwaacha Barca na Real wakiwa na pointi 87 kila moja. Atletico watakipiga tena wikiendi ijayo na Real Madrid katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Katika hatua nyingine, Juventus wa Italia wameweka rekodi mpya katika ligi 10 bora barani kwa kufikisha pointi 102.
Juve wamemaliza ligi kwa kuwa mabingwa wakiwa na pointi 17 zaidi ya Roma walioshika nafasi ya pili. Juve wameshinda mechi zao zote 19 za nyumbani.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Taifa Stars yaichapa Zimbabwe 1-0

Washabiki Arsenal wafunika mitaa