in , ,

Arsenal wapotea njia

 

Matumaini ya Arsenal kutwaa ubingwa katika Ligi Kuu ya England (EPL)

msimu huu yaliyokuwa yameanza kuwa makubwa yamezidi kupotea baada ya

kupoteza mechi muhimu dhidi ya Manchester United.

Kijana mwenye umri wa miaka 18, Marcus Rashford wa United alifunga

mabao mawili wakicheza nyumbani Old Trafford, kwenye mechi

iliyomalizika kwa Man U kushinda 3-2. Arsenal walianza kwenda vibaya

kwa kufungwa na Chelsea, kabla ya kutibuliwa pia na Barcelona kwenye

mechi ya mkondo wa kwanza ya 16 bora katika Ligi ya Mabingwa Ulaya

(UCL) nyumbani Emirates; wlaifungwa 2-0.

Arsenal wanaonekana bado kujiamini, kwani kwenye mechi dhidi ya

Barcelona wiki jana, walicheza vyema lakini wakashindwa kutumia vizuri

fursa kadhaa walizopata na wangeweza kuibuka na ushindi.

Wakati wakitazamwa na wengi, shinikizo pia likiwa kwao ili waweze

kupanda na kuwakuta vinara wa ligi – Leicester na wapinzani wao wa

London Kaskazini – Tottenham Hotspur, walishindwa kuondoka walau na

pointi moja ugenini Jumapili hii.

Rashford alianzishwa na kocha Louis van Gaal dhidi ya timu ya FC

Midtjylland Alhamisi kwenye mechi ya Kombe la FA na akafunga mabao

mawili. Mchezaji wa zamani wa Man U, Danny Welbeck naye aliwazodoa

Mashetani Wekundu kwa kuwafunga tena, lakini Ander Herrera aliwafunga

Arsenal. Mesut Ozil alirejesha matumaini kwa kupachika bao lakini

United walisimama imara hadi mwisho na kushinda mechi hiyo.

Arsenal hawajatwaa ubingwa tangu 2004, na kwa matokeo ya Jumapili hii

wanabaki nafasi ya tatu wakiwa na pointi tano pungufu ya vinara na

tatu nyuma ya Spurs. Man U wamepanda hadi nafasi ya tano, wakiwa na

ushindi wa kwanza katika mechi tatu za EPL.

United walikuwa na kikosi cha vijana bila wazoefu wengi na Arsenal

walishindwa kutumia fursa hiyo kuonesha wana nia kweli ya kutwaa

ubingwa. Leicester walipata ushindi mwembamba dakika za mwisho dhidi

ya Norwich na Spurs wakawashinda Swansea ikimaanisha Arsenal wana kazi

ngumu zaidi.

Kocha Arsene Wenger ameshuhudia timu yake ikiyumba kwenye mashindano

matatu tofauti, kwani walitoshana nguvu na Hull kwenye michuano ya

Kombe la FA, hivyo kuwa na mechi moja ya ziada; kwa ajili ya marudiano

kujua iwapo wataingia robo fainali au la. Hili linaweza pia

kuwaongezea majeruhi.

Wakati kaimu nahodha msaidizi wa klabu hiyo, Per Mertesacker alisema

tatizo lao kubwa ni kwenye ushambuliaji, mambo yalikuwa tofauti

Jumapili hii na Wenger alilalamika jinsi walivyokubali mabao mawili

marahisi kufungwa. Mertesacker alikuwa benchi, nafasi yake

ikachukuliwa na Gabriel.

Mechi ijayo Arsenal watacheza na Swansea, wakati United watapepetana

na Watford walio katika nafasi ya 10.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

Leicester mbele kwa mbele

Tanzania Sports

Man City watwaa Kombe la Ligi