in ,

Arsenal mtihani mpya FA

Mabingwa watetezi wa Kombe la FA, Arsenal wamebanwa na Hull kwenye

mechi ya 16 bora kwa kwenda suluhu.

Katika mechi ambayo Arsenal walitawala kwa kila hali wakicheza

nyumbani, kikwazo kikubwa kilikuwa kipa wa Hull, Eldin Jakupovic.

Kwa matokeo hayo, Arsenal watatakiwa kusafiri kwenda kucheza na Hull

nyumbani kwao katika mechi ambayo, lazima, mshindi atapatikana.

Washika Bunduki wa London waliona kwamba walikataliwa penati mbili

ambazo huenda zingewapa ushindi, kutokana nakuchezewa vibaya kwa Theo

Walcott na Danny Welbeck waliotoka kwenye majeruhi hivi karibuni.

Timu inapata tabu ya kupata ushindi, inapocheza na timu dhaifu
Timu inapata tabu ya kupata ushindi, inapocheza na timu dhaifu

Kipa Jakupovic aliwaokoa Hull ambao walionekana wangesalimu amri kama

walivyofanya msimu uliopita kwenye mashindano kama haya. Moja ya hayo

ni kutungua mpira wa adhabu ndogo wa Joel Campbell ukaishia kugonga

mwamba.

The Tigers, jina jingine la Hull, walitengeneza nafasi chache za

kufunga lakini walilinda lango lao na kumweka katika hali ngumu kocha

Arsene Wenger aliyekuwa akiwaongoza Arsenal katika mechi yake ya 100

kwenye michuano hii akiwa bosi wao.

Hull wanaofundishwa na Steve Bruce na ambao wanaongoza Ligi Daraja la

Kwanza (Championships) nao hawakufurahia matokeo, kwani wamekatizwa

mserereko wa ushindi katika mechi 14 zilizopita.

Timu mbili hizi zilikutana kwenye fainali ya Kombe la FA 2014 na

raundi ya tatu msimu uliopita; zote Arsenal wakishinda.

Ni wazi kwamba kipaumbele kwa Arsenal kipo kwingine, wakiwa pointi

mbili tu nyuma ya Leicester wanaoongoza Ligi Kuu ya England (EPL).

Jumanne hii wana kibarua kingine cha kuwakaribisha Barcelona katika

mechi ya mkondo wa kwanza ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL).

Arsenal hawajapata kuvuka hatua hii katika misimu mitano iliyopita, na

katika mechi dhidi ya Hull, mchezaji wao muhimu katika kutengeneza na

kufunga mabao, Mesut Ozil alipumzishwa, wakati Olivier Giroud na

Alexis Sanchez ambao ni muhimu pia walianzia benchi hadi dakika za

mwisho mwisho.

Hii ni mara ya kwanza kwa Hull kutoruhusu Arsenal kuwafunga walau bao

moja katika mechi 17 walizokutana kwenye mashindano yote, na mara ya

mwisho ilikuwa 1915. Jumamosi hii Arsenal walipiga mashuti 24 ambayo

hayakuzaa bao lolote, mengi kuliko mechi yoyote msimu huu katika

mashindano yote.

Katika mechi nyingine, Reading waliwakandamiza West Bromwich Albion

kwa mabao 3-1 na kuvuka, Watford wakapoteza 0-1 kwa Leeds wakati

Bournemouth wakazidiwa nguvu 0-2 na Everton.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

YANGA YAUA MNYAMA, YAREJEA KILELENI.

Tanzania Sports

Chelsea wawaogesha Man City