in , , ,

Arsenal, Chelsea nguvu sawa

 

*Man United wapigwa tatu bila

 

Mtanange mkubwa katika Jiji la London umemalizika kwa suluhu baina ya Arsenal na Chelsea.

 

Kama ilivyotarajiwa, Chelsea walijilinda zaidi kuliko kushambulia na Arsenal walikosa nafasi kadhaa katika kipindi cha pili.

 

Washabiki wa Arsenal waliwazomea Chelsea wakisema kwamba walikuwa wakifanya mchezo udorore kwa jinsi walivyokuwa wakibana nyuma, lakini kocha wao, Jose Mourinho alidai walitoa somo juu ya ulinzi.

 

Wachezaji wa Chelsea walishangilia suluhu hiyo kana kwamba walikuwa wameshinda, hasa nahodha wao, John Terry.

 

Arsena sasa hawajaweza kuwafunga Chelsea katika mechi 13 dhidi ya Mourinho na sasa Chelsea wanakaribia kuutwaa ubingwa wa England, wakati Arsenal wakianguka hadi nafasi ya tatu.

 

 

 

MANCHESTER UNITED HOI

gea

 

Manchester United kwa upande mwingine waliangukia pua mbele ya Everton kwa kukung’utwa 3-0 kwenye dimba la Goodison Park.

 

Vijana wa Louis van Gaal walishindwa kabisa kufanya vyema mchezoni wakacharazwa kama wamesimama.

 

Mabao ya wenyeji yalifungwa na James McCarthy, John Stones na Kevin Mirallas, ambayo yangeweza kuzuilika kama Mashetani Wekundu wangelinda vyema.

 

Huu ulikuwa ushindi mkubwa zaidi wa Everton dhidi ya Manchester United katika muda wa miaka 23.

 

MATOKEO MENGINE YA LIGI KUU

table

 

 

Katika mechi nyingine za wikiendi hii, Manchester City walipata ushindi wa 3-2 dhidi ya Aston Villa na kupanda hadi nafasi ya pili lakini wana mechi moja zaidi ya Chelsea na Arsenal.

 

Southampton walikwenda sare ya 2-2 na Tottenham Hotspur, Burnley wakalala kwa Leicester, Crystal Palace wakalala 2-0 kwa Hull na Newcastle wakalala 2-3 mbele ya Swansea.

 

Kwenye mechi nyingine Queen Park Rangers (QPR) walikwenda suluhu na West Ham, Stoke wakatoka sare ya 1-1 na Sunderland na West Bromwich Albion wakawalazimisha suluhu Liverpool.

 

Kwa matokeo hayo, Chelsea wanaongoza ligi kwa alama 77 wakifuatiwa na Man City wenye 67 sawa na Arsenal wakati Man United wanazo 65.

 

Liverpool wanashika nafasi ya tano kwa alama 58 sawa na Spurs wakifuatiwa na Southampton wenye 57.

 

Swansea, Stoke na Everton wanafunga 10 bora wakati Burnley wapo mkiani na alama 26, QPR wanazo 27 na Sunderland 30 hivyo kuwa katika hatari ya kushuka daraja.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Manchester United mapambano

MALINZI AFUNGUA KOZI YA WAKUFUNZI