in , , ,

RAUNDI YA TANO KOMBE LA FA:

 

Ni Chelsea vs Man City

HATIMAYE ratiba ya mechi za raundi ya tano kuwania Kombe la FA

imetoka, ambapo Chelsea watawakaribisha Manchester City.

Kombe hilo linashikiliwa na Arsenal kwa msimu wa pili mfululizo,

ambapo pia safari hii wamefuzu kwa raundi hii ya 16 bora.

Ratiba hii inamaanisha kwamba ama Chelsea au City watalikosa kombe

hili la pili kwa ukubwa nchini England baada ya lile la Ligi Kuu

(EPL).

Mechi hizi zitakazochezwa kati ya Februari 19 na 22, zinakuja wakati

Chelsea wakielekea kuanza kuimarika wakiwa na kocha Guus Hiddink,

baada ya kuanza msimu vibaya na kocha aliyefutwa kazi, Jose Mourinho.

Chelsea na City walikutana Agosti mwaka jana kwenye mechi ya EPL,

ambao City walishinda kwa 3-0.

Timu inayocheza kwenye League One, Shrewsbury Town, wanaochukuliwa

kuwa vibonde zaidi miongoni mwa klabu zilizofuzu watawakaribisha

Manchester United kwenye dimba la New Meadow.

Mabingwa watetezi, Arsenal, watapepetana na Hull, ikiwa ni kama

marejeo ya fainali ya 2014, ambapo Arsenal walishinda na kujifariji

sana kwa taji hilo.

Ratiba hiyo inaonesha kwamba Crystal Palace watakuwa wageni wa

Tottenham Hotspur, wakati Bournemouth watawakaribisha Everton katika

mechi zinazokutanisha timu za ligi kuu.

Mechi nyingine zitashuhudia Watford wakikamatana na Leeds United;

Reading watakabiliana na mshindi kwenye mechi ya marudiano baina ya

West Bromwich Albion.

Peterborough na Blackburn watacheza na ama Liverpool au West Ham

kulingana na matokeo ya mechi za marudio.

Mechi ya kuvuta wengi zaidi ni baina ya mabingwa wa karibuni zaidi wa

EPL, ambapo Hiddink ameshasema kwamba hiyo ni “huge game” –

itakayovuta watu wengi zaidi, akisema tayari ni kama fainali, maana

mmoja lazima aachie ngazi.

Hii ni droo ya tatu mfululizo dhidi ya timu ya EPL kwa kikosi cha

Manuel Pellegrini wakati Arsenal wanakutana na Hull kwa mara ya tatu

katika misimu mitatu. Mwaka jana Washika Bunduki wa London

waliwashinda Hull 2-0 katika raundi ya tatu mwaka jana.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

Simba yazidi kutakata..VPL

Tanzania Sports

Mamia ya wanafunzi wajiunga na PSPF