in , , ,

Simba yatokelezea vilivyo


*Yanga wamemrejesha Chuji, Kiiza naye fiti
*Barcelona wapigwa nyumbani Nou Camp

Wekundu wa Msimbazi, Simba wamesafisha mwezi kwa kuwakandika maafande wa Oljoro JKT mabao 4-0 huku wakiwasikilizia wapinzani wao Yanga leo.
Mabao ya Simba kwenye mechi hiyo iliyopigwa Uwanja wa Taifa yalifungwa na Amisi Tambwe aliyepiga na hat-trick na kuondoka na mpira, akisema hakutarajia kufunga mengi hivyo.
Bao jingine la Simba lilifungwa na Jonas Mkude na jitihada za Oljoro kutumia mbinu za kiraia na kijeshi chini ya kocha Hemed Morocco hazikufanikiwa hata kidogo.

YANGA NA MBEYA, CHUJI, KIIZA WARUDI

Wakati Simba wakishinda Jumamosi hii, vijana wa makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Yanga Jumapili hii wana kipute dhidi ya Mbeya City.
Hadi watakapoingia uwanjani Jumapili hii, Mbeya City wanajivunia kwa kutofungwa mechi yoyote tangu kuanza kwa Ligi Kuu ya Tanzania.
Kocha Juma Mwambusi anasema anawajua Yanga ni timu kubwa, anawaheshimu pia kwa sababu ni mabingwa watetezi lakini kwamba hata wao Mbeya wana heshima na anaamini mchezo utakuwa mgumu.
Yanga walikwenda Bagamoyo kujiandaa kwa mechi hiyo baada ya kutoka suluhu mjini Tanga walikocheza na Coastal Union.
Kadhalika waliamua kumrejesha kundini kiungo mahiri Athumani Idd Chuji huku mshambuliaji matata Mganda, Hamisi Kiiza naye akiwa pia amerejea. Itakuwa juu ya benchi la ufundi kuona kama wacheze au la.

BARCELONA WACHAPWA NYUMBANI

Mabingwa wa Hispania, Barcelona wamepoteza mechi katika uwanja wao wa nyumbani wa Nou Camp kwa mara ya kwanza tangu Aprili 2012.
Jumamosi hii ilikuwa chungu jijini hapo, pale Valencia walipomaliza ubishi wao, huku nyota wa Barca, Lionel Messi na wengine wakiwa ndani. Valencia walikatisha ushindi wa mechi 25 mfululizo katika dimba hilo kubwa na la aina yake.
Valencia pia wanakuwa timu ya kwanza kufunga mabao matatu katika mechi ya ushindani hapo Nou Camp dhidi ya kikosi cha Gerardo Martino. Mabao ya Barca yalifungwa na Alexis Sanchez wakati Messi alifunga kwa penati.
Valencia walipata mabao yao kupitia kwa Parejo, Piatti na Alcácer García .
Barca walimaliza wakiwa 10 baada ya Jordi Alba kuzawadiwa kadi nyekundu kwa rafu mbaya dhidi ya Sofiane Feghouli dakika 13 kabla ya mchezo kumalizika.
Mara ya mwisho Barca kufungwa Camp Nou ni Aprili 2012 walipopoteza mechi kwa wapinzani wao wakubwa nchini humo, Real Madrid kwa mabao 2-1.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Aragones: Siri ya mafanikio Hispania

Arsenal warudi kileleni