in , , ,

Kicheko Chelsea, Spurs

Mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya England (EPL) umeendelea kwa kicheko kwa klabu mbili za London.
Chelsea wanaotoka upande wa magharibi walifurahia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya timu mpya iliyopanda daraja ya Hull wakati Tottenham Hotspur wa London Kaskazini waliwashinda wageni wengine Crystal Palace kwa bao 1-0 la tuta.
Vijana wa Jose Mourinho walipata mabao yao kupitia kwa Oscar na Frank Lampard katika nusu ya kwanza ya mchezo, na kumhakikishia Mourinho marejeo mema.

20130729-213015.jpg

Lampard, hata hivyo, anayeaminika sana kwa kufunga penati, alikosa katika mkwaju wake wa kwanza msimu huu, kwani uliokolewa na kipa Allan McGregor, kabla ya Kevin de Bruyne kumtengea Oscar pande lililoleta bao.
Alikuwa McGregor tena aliyesababisha bao la pili, ambapo Lampard ambaye ni kiungo wa timu ya taifa ya England, alifunga kwa mkwaju wa adhabu ndogo.
Kipindi cha pili Hull walionekana kujitahidi kuwakabili Chelsea ili kurejesha mabao na pengine kupata ushindi, lakini hawakuwa na uwezo huo.
Mourinho akizungumzia ushindi huo, alisema kwamba alikuwa mahali pake, uwanja wake na kwa watu wake.
Kwa upande wa vijana wa Andre Villas-Boas, walipata bao lao la ushindi kwa mkwaju wa penati uliopigwa na mchezaji mpya, Roberto Soldado aliyevunja rekodi ya klabu kwa kusajiliwa kwa pauni milioni 26 kutoka Valencia ya Hispania.
Penati hiyo ilitolewa baada ya majalo ya Aaron Lennon kushikwa na beki Dean Moxey. Hata hivyo, kocha wa Crystal Palace, Ian Holloway alieleza kutoridhishwa na jinsi waamuzi walivyochezesha pambano hilo.
Spurs walicheza bila nyota wao, Gareth Bale anayetakiwa na Real Madrid, kwani inadaiwa kwamba ana majeraha ya mguu.
Inaweza kuwa mapema sana kutoa msimamo wa ligi, lakini mabingwa watetezi Manchester United wanaongoza kwa kuwa na pointi tatu, lakini wanawazidi mabao na kwa mpangilio huu washindani wao; Aston Villa, Chelsea, West Ham, Fulham, Liverpool, southampton na Spurs.

Enhanced by Zemanta

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

25 WACHUKUA FOMU UCHAGUZI TFF

U20 WANAWAKE KUANZIA RAUNDI YA KWANZA KOMBE LA DUNIA