in , , ,

Manchester United safi ukuzaji vipaji

*Barcelona waongoza barani Ulaya
*Klabu za Ufaransa nazo zajivunia

 

Manchester United ni miongoni mwa klabu zinazowika zaidi England kwa kuzalisha chipukizi bora wanaotamba kwenye soka barani Ulaya.
Man United wanaounyemelea ubingwa wa England walioupoteza mwaka jana, wana jumla ya wachezaji 24 wanaotamba katika ligi tano za madaraja ya juu kabisa barani.
Kadhalika, United wanaofundishwa na Alex Ferguson tangu mwaka 1986 wana nyota tisa katika kikosi kinachoshiriki Ligi Kuu ya England (EPL), walioanzia kwenye shule yao.
Hao wanatofautiana kwa umri na uzoefu, kutoka Ryan Giggs hadi Danny Welbeck na Tom Cleverly walio na kikosi cha kwanza.
Hata hivyo, klabu inayotoa nafasi kwa chipukizi zaidi katika timu yao kwa sasa ni Athletic Bilbao, yenye wachezaji 16 waliokaa klabuni hapo kwa walau miaka mitatu wakiwa na kati ya umri wa miaka 15 na 21.

20130328-091057.jpg
Bilbao wanatambulika kwa wingi wa wachezaji kutka eneo la Basque na sera yao ya ‘Cantera’.
Barcelona wanafuatia, wakitamba na shule yao ya mafunzo maarufu kwa jina la ‘La Masia’ iliyozalisha wachezaji 14 wanaochezea timu ya wakubwa.
Hao ni pamoja na Xavi, Andres Iniesta na Lionel Messi wakati Real Sociedad (kutoka eneo la Basque pia) wakiwa na idadi hiyo hiyo ya wachezaji waliokuzwa, lakini wenyewe ni katika jimbo la Guipuscoa.
Manchester United ndiyo klabu pekee ya Uingereza miongoni 10 bora katika kukuza vipaji, ikiungana pia na klabu za Ufaransa – Montepellier, Sochaux-Montpeliard, Lyon na Bordeaux, wakionesha umahiri wao katika kukuza vipaji.
Klabu hii ya Ferguson inajivunia rekodi ya nne bora zaidi miongoni mwa klabu katika ligi tano bora za Ulaya – Premier League, La Liga, Serie A, Bundesliga na Ligue 1.
Inaheshimika kwa jinsi inavyokuza wachezaji na kuwawezesha kubaki kwenye klabu yao, au kupata ajira kwenye ligi nyingine bora barani Ulaya.
Wanaoongoza njia katika ukuzaji vipaji barani Ulaya ni Barcelona wenye wachezaji 38 waliozalishwa na La Masia wanaotamba kwenye ligi bora barani Ulaya.
Lyon ya Ufaransa inao 32 wakati Real Madrid inatambia wachezaji wake 29.

20130328-091110.jpg
Unyakuaji wa wachezaji kutoka Bernabeu unazidi kuinyima Real Madrid vipaji vyake, ambapo waliosajiliwa kutoka hapo ni pamoja na kiungo wa Chelsea, Juan Mata, Javi Garcia wa Manchester City na mshambuliaji wa Sevilla, Alvaro Negredo waliotokana na kituo cha mafunzo cha Castilla cha Real Madrid.
Pamoja na simulizi za siku nyingi juu ya Arsenal na kocha wao, Arsene Wenger kuwa maarufu kwa kukuza vipaji, wanao wachezaji sita tu waliotengenezwa hapo, lakini wengine 14 waliruhusiwa kujiunga na mahasimu wa klabu kwenye ligi mbalimbali Ulaya.

 

 

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Safari ya Brazil, Zimbabwe yatolewa jasho na Misri

Abou Diaby: Jembe lililovunjika mpini