in , , ,

Wembley: Fainali Euro 2016

England watakuwa wenyeji wa fainali zijazo za Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL) na mechi itapigwa kwenye Uwanja wa Wembley.

Shirikisho la Soka la Ulaya (Uefa) limetangaza rasmi kwamba Chama cha Soka cha England (FA) kimeshinda kwenye maombi yaliyowasilishwa ya kuwa mwenyeji. Tayari mechi za mkondo wa kwanza kwenye makundi zimechezwa.

Wembley ndio uwanja unaotumiwa kama wa taifa kwa England, ambapo huchezewa mechi za kimataifa na nyingine kwa kadiri FA inavyopanga, kama fainali za Kombe la FA na mechi nyingine kubwa.

Uefa imesema kwamba viwanja vya Hampden Park uliopo Uskochi na Aviva uliopo Dublin nchini Ireland vitatumika kwa ajili ya mechi 16 za mwisho na tatu za hatua ya makundi.

FA ya England imeishinda ile ya Ujerumani (DFB) waliotaka kuwa wenyeji, na badala yake watafanya hivyo katika moja ya hatua za robo fainali na mechi tatu za makundi kadhalika.

Mechi za robo fainali na mechi tatu za makundi zitachezwa Munich (Ujerumani), Baku (Azerbaijan), Roma (Italia) and St Petersburg nchini Urusi.

Majiji wenyeji yatakayoandaa mechi tatu za makundi katika hatua ya 16 bora ni Copenhagen (Denmark), Bucharest (Romania), Amsterdam (Uholanzi), Bilbao (Hispania), Budapest (Hungary) na Brussels nchini Ubelgiji.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Wachezaji wa kigeni kupunguzwa

Ozil, Welbeck wawang’arisha Arsenal