in , ,

Tanzania yapokelewa rasmi madola

Timu ya Tanzania

Timu ya Tanzania inayoshiriki michezo ya Jumuia ya Madola Glasgow 2014 leo alasiri impokelewa rasmi katika kijiji cha michezo hapa Glasgow Scotland.

Katika sherehe hiyo fupi ilioandamana na kupandishwa kwa bendera na kupigwa wimbo wa taifa ulijumuisha wanamichezo 40 wakiwemo Watanzania waishio hapa, pamoja   na viongozi.

Sherehe hizo zilizofana sana  pia zilihudhuriwa na Afisa ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza Ndugu Amos Msanjila.

Wakati huo huo Naibu waziri wa Habari Utamaduni na Michezo Ndugu Juma Nkamia kesho asubuhi anatarajia kutembelea wanamichezo wa Tanzania hapa kijiji cha michezo.

Pamoja na Naibu waziri wengine wanao taraji kufuatana naye ni Rais wa Kamati ya Olimpiki nchini Ndugu Gulam Abdallah na Katibu mkuu wa TOC ndugu Filbert Bayi.

Michezo inataraji kufunguliwa rasmi siku ya Jumatano na Malkia wa Uingereza katika sherehe zinazotarajiwa kuanza saa tatu usiku.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Nahodha Ujerumani aachia ngazi

Sare siyo mbaya- Nooij