in , ,

Rudisha ashinda mbio Uingereza

Mkenya David Rudisha amerejea katika makali yake kwa kutwaa ubingwa katika mbio za mita 800 za Diamond League jijini Glasgow, Scotland.
Hii ni mara ya kwanza kwa raia huyu wa Afrika Mashariki kupata ushindi katika ardhi ya Uingereza tangu alipopata medali ya dhahabu kwenye mbio za London 2012.

Rudisha (25) alikuwa nje kidogo kutokana na majeraha lakini sasa ameweka rekodi ya dunia kwa kuwatangulia wenzake kwa dakika nzima, akikimbia dakika 1:43.34.

“Najihisi mwenye furaha kubwa sana kwa sababu nipo vizuri sasa baada ya kuwa na mwaka mgumu lakini sasa nimejiweka sawa ndio maana nilikimbia kwa kasi kubwa,” anasema Rudisha ambaye atakuwa tena Hampden Park kwa ajili ya michuano ya Jumuiya ya Madola baadaye mwezi huu.

Nafasi ya pili ilichukuliwa na Andre Olivier wa Afrika Kusini huku mshindi wa medali ya dhahabu wa Marekani, Allyson Felix na Mjamaica Shelly-Ann Fraser-Pryce walifuatia, nao wakiwa pia wanatoka kwenye majeraha.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Brazil sikio la kufa

UJERUMANI NI BINGWA, LABDA ITOKEE MIUJIZA KWA ARGENTINA