in , , ,

Newcastle hali tete

Kocha wa Newcastle, Alan Pardew ametiwa katika shinikizo jipya baada ya kuendelea kupoteza mechi.

Washabiki wa Newcastle wamekuwa wakimtaka mmiliki wa klabu, Mike Ashley kumfukuza kocha huyo, kwani timu imo mkiani mwa ligi na hakuna jipya.

Mmiliki huyo alidai kabla ya mechi dhidi ya Stoke kwamba angemfuta kazi Pardew iwapo wangepoteza mechi, lakini baada ya Stoke kuwafunga 1-0, akadai ilikuwa utani tu.
Washabiki waliendelea kubeba mabango yenye maandishi ya kutaka kufukuzwa kwa kocha huyo Mwingereza, mengine yakiwa na picha yake ikifananishwa na katuni tata.
Ujumbe mwingine ulikuwa kwamba wana imani na timu ila kocha hawezi na wengine wakiandika kwamba tatizo la klabu yao ni mmiliki, Ashley.

Bao la kichwa la Peter Crouch limemwelekeza pabaya kocha huyo, ambaye lolote sasa linaweza kumpata, ama kufukuzwa, mwenyewe kung’atuka au kuendelea kuzongwa na washabiki.

Newcastle wanashika nafasi ya 20 miongoni mwa idadi hiyo ya timu kwenye msimamo wa ligi, wakiwa na pointi tatu kutokana na mechi sita, sawa na Burnley, huku uwiano wa mabao kwa timu zote mbili ukiwa ni -7.

Pardew aliwaambia waandishi wa habari kwamba ataendelea na kazi yake, wala hana mpango wa kujiuzulu, japokuwa shinikizo likizidi ataondoka tu.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Chelsea wajidai kileleni

Chelsea safi, Man City wabanwa