in , , , ,

Mourinho amtishia Hazard

*Guardiola hajui hatima yake

Matokeo mabaya kwenye nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL) yamewachanganya makocha wa Chelsea na Bayern Munich.

Wakati Jose Mourinho wa Chelsea akimalizia hasira zake kwa mchezaji kinda na mahiri, Eden Hazard kwa kumchagiza, Pep Guardiola amesema kwamba Bayern wanatakiwa kutafakari iwapo yeye ndiye anafaa kuwa kocha wao.

Hazard alimbwatukia kocha wake kwa mbinu zake na sasa Mourinho amemtishia huku akisema kwamba winga huyo bado hajaanza kujituma kabisa kwa ajili ya klabu yake.

Inaelezwa kwamba Paris Saint-Germain wa Ufaransa wanamwania Hazard kwa ajili ya msimu ujao na ndiye amekuwa nguzo muhimu kwa Chelsea lakini timu hiyo ya London ilifungwa 3-1 na Atletico Madrid Uwanja wa Stamford Bridge na kuwachukiza washabiki wa Chelsea.

Mourinho anasema kwamba Hazard alifanya makosa kwenye mechi hiyo na kuruhusu bao la kwanza na kusema ni aina ya wachezajiw asiotoa suluhu ya tatizo bali wanalaumu tu.

Katika hatua nyingine, Guardiola amesema kwamba ni juu ya Bayern kuamua hatima yake. Bayern walifungwa 4-0 na Real Madrid.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Ubingwa Ulaya waenda Hispania

Man City washindwe wenyewe