in , ,

Mo Farah ajitoa Madola

Mwanariadha mashuhuri wa Uingereza mwenye asili ya Somalia, Mo Farah amejitoa kwenye michuano ya Jumuiya ya Madola inayofanyika Glasgow, Scotland.

Farah alikuwa akimbie katika mbio za meta 5,000 na 10,000 lakini amekwama baada ya kuugua, ambapo amesema mwili wake haupo fiti kwa kazi hiyo.

Kujiondoa kwa Farah ambaye kwenye michezo ya Olimpiki iliyofanyika England alitwaa medali mbili za dhahabu ni pigo kwani ni mmoja wa wachezaji mahiri waliotarajiwa kuipamba.

Farah amesema kwamba hivi sasa anajiandaa kwa ajili ya michuano ya Ulaya iliyopangwa kufanyika Agosti mwaka huu.

Farah alijitoa pia katika michuano ya Diamond League majuzi na sasa ameikosa ya Glasgow baada ya kulazwa hospitali kwa siku mbili akilalamika kwamba ana maumivu ya tumbo.

Hadi jana England ilikuwa inaongoza kwa kutwaa medali sita za dhahabu, saba za fedha na nne za shaba, ikifuatiwa na Australia wenye tano za dhahabu, tatu za fedha na saba za shaba.

Wenyeji Scotland nao hawapo vibaya, kwani hadi jana walikuwa wametwaa medali nne za dhahabu, tatu za fedha na tatu pia za shaba.

Afrka Kusini Ghana na Nigeria ndizo zilizochomoza kwa upande wa Afrika, ambapo Afrika Kusini ina mbili za shaba na Ghana wana moja moja.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

MASHINDANO YA JUMUIYA YA MADOLA YAMEPOTEZA MVUTO

Drogba arudi Chelsea