in ,

KAGERA SUGAR KUHAMA UWANJA

Timu ya Kagera Sugar ambayo inashiriki ligi Kuu ya Vodacom imeamua kuhama Uwanja wa CCM Kirumba uliopo Mwanza na timu hiyo itahamia Uwanja wa Kambarage Uliopo shinyanga.

kocha Msaidizi wa Kagera sugar Mrage Kabange alisema watahama Uwanja wa CCM Kirumba na Mechi zake zote za raundi ya pili zitachezwa Uwanja wa Kambarage ulipo shinyanga.

“Uwanja wa CCM Kirumba umetukataa Kabisa na Hatuna Bahati Nao tumecheza mechi 3 na zote tumepoteza” Kabange alisema
Kagera ilicheza na Azam ikafungwa 3-1,Mbeya city Ilimpiga Kagera1-0,Ndanda Imemfunga Kagera 2-1.Mechi zote zilichezwa CCM KIrumba.

Kocha Mkuu wa Kagera sugar Jackson Mayanja Ameenda Kusoma Mafunzo ya ukocha ya juu mjini Kampala,Uganda na atarudi Nchini Tarehe 5 feb.

Licha ya Uwanja pia Kagera sugar inakabiliwa na tatizo la Majeruhi kwa wachezaji wake ambao ni Benjamin Askwire,Malegesi Mwanga,Dickson Mbada,Yusuph Komba na Salum Kanoni.
Pia Kagera Sugar Haipati Mashabiki wengi Kwakuwa Inachukiwa na Watu wa Mwanza kwakuwa Kagera sugar ndio iliyosababisha Toto African ya Mwanza Kushuka Daraja.

Kagera sugar hapo awali ilikuwa ikicheza Mechi zake katika Uwanja wake wa Nyumbani wa kaitaba.Mpaka sasa uwanja wa kaitaba upo katika Matengenezo ya kuweka Nyasi bandia.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Ghana, Ivory Coast nusu fainali AFCON

Juan Quadrado atua Chelsea