in , , ,

Ferguson huyoo Harvard

Kocha aliyestaafu Manchester United, Sir Alex Ferguson amejiunga na Chuo Kikuu cha Harvard ambako alikoingia mkataba wa kufundisha kwa muda mrefu.

Ferguson (72) ataanza kazi yake hiyo mpya mapema mwezi ujao katika programu mpya chuoni hapo inayohusu Biashara, Burudani, Vyombo vya Habari na Michezo katika moja ya vyuo vinavyoheshimika zaidi duniani.

Fergie ndiye kocha aliyepata mafanikio makubwa zaidi nchini Uingereza na alifikia makubaliano ya kazi hiyo nchini Marekani, na anatarajiwa kurejea huko mwezi ujao kwa ajili ya kutoa mhadhara kwa maofisa watendaji waandamizi kutoka maeneo mbalimbali duniani.

Mskochi huyo ameona ni bora kuchukua kazi hiyo badala ya kuendelea kuketi kwenye jukwaa la watu maarufu au viongozi kutazama timu yake aliyomwachia David Moyes inavyofanya kazi. Alikaa Old Trafford kwa miaka 26 yenye mafanikio makubwa.

“Nimefurahishwa sana kupata fursa kama hii ya kuchangia nilicho nacho katika chuo chenye sifa kubwa miongoni mwa wasomi duniani. Muda niliokaa hapa tayari umenichochea uzoefu wangu na natumaini kuendeleza uhusiano mzuri katika shughuli za wanafunzi, vitivo na marafiki katika chuo hiki,” akasema Fergie akiwa Marekani.

Ferguson aliwawezesha Man U kutwaa jumla ya vikombe 38, kati ya hivyo 13 vikiwa ni vya ubingwa wa ligi kuu, viwili vya Ligi ya Mabingwa Ulaya na pia kuna vingine vya mashindano tofauti ndani na nje ya nchi. Kwa sasa ni balozi na mmoja wa wakurugenzi wa klabu hiyo.

Profesa wa Harvard, Anita Elberse amesema wamefurahishwa na Fergie kukubali kuchukua jukumu hilo jipya na kwamba wanasubiri kwa hamu ili aianze rasmi kazi yake hiyo, ambapo watapata uzoefu wake kwenye uongozi.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Tanzania Kucheza Nusu fainali ya Kombe la Dunia la Watoto wa Mitaani, Brazil…

Rooney aumia, kukosa mechi