in , , ,

Di Matteo kocha mpya Schalke

 
Klabu ya Ujerumani ya Schalke wamemteua kocha wa zamani wa Chelsea na West Bromwich Albion, Roberto Di Matteo kuwa kocha wao.

Di Matteo (44) anachukua nafasi ya Jens Keller kutokana na timu ya klabu hiyo kuanza vibaya msimu wa Bundesliga mwaka huu.

Schalke wanashika nafasi ya 11 kwenye msimamo wa ligi kuu nchini mwao, wakiwa na pointi nane tu kutokana na mechi saba, ambapo wameshinda mara mbili tu.

Katika Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL), Schalke wanashika nafasi ya tatu, ambapo walipocheza Stamford Bridge walikwenda sare ya 1-1 na Chelsea.
Di Matteo atawaongoza Schalke dhidi ya klabu yake hiyo ya zamani kwenye mechi ya marudiano nchini Ujerumani Novemba 25.

Keller alikuwa bosi wa Schalke tangu Desemba 2012, lakini walitolewa kwenye Kombe la Ujerumani na SG Dynamo Dresden walio daraja la tatu mapema msimu huu na mechi yake ya mwisho alishuhudia wakifungwa
2-1 na Hoffenheim wikiendi iliyopita.

Hii ni kazi ya kwanza ya Di Matteo tangu alipofukuzwa kazi na Chelsea Novemba 2012. Alichukua nafasi hiyo kama kaimu pale Chelsea walipomfukuza kazi Andre Villas-Boas Machi 2012.

Aliwaongoza Chelsea kutwaa ubingwa wa Ulaya na Kombe la FA na kupewa ukocha wa kudumu lakini msimu uliofuata walikwenda vibaya, akafukuzwa na nafasi yake kuchukuliwa na Rafa Benitez kwa mpito hadi Jose Mourinho aliporejea msimu uliopita kutoka Real Madrid.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Chelsea hawakamatiki

Muhammad Ali hoi kitandani